Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Isaya 51:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Kati ya watoto wote uliowazaa hakuna yeyote wa kukuongoza. Hakuna hata mumoja wa kukushika mukono kati ya watoto wote uliowalea.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Isaya 51:18
18 Σταυροειδείς Αναφορές  

Sikia! Mungu hatakataa mutu mukamilifu, wala hatasaidia waovu.


Roho yangu inaporegea kabisa, yeye yuko, anajua mwenendo wangu. Waadui wamenitegea mitego katika njia ninayopita.


Yananizunguka kama mafuriko muchana kutwa; yananizunguka yote pamoja.


Mimi ndiye Yawe, Mungu wako, ndiye ninayeshika mukono wako. Mimi ndiye ninayekuambia: Usiogope, nitakusaidia.


Yawe anasema hivi kwa Kiro, muchaguliwa wake: Nilikuchagua kuwa mufalme kwa kunitumikia. Ninaimarisha nguvu yako kusudi uyashinde mataifa mbele yako, na kuzivunja nguvu za wafalme. Mimi ninafungua milango ya muji mbele yako, na hakuna mulango utakaofungwa.


Kwa hiyo utajiuliza mwenyewe: Nani aliyenizalia watoto hawa wote? Nilikufiwa na watoto bila kupata wengine. Nilipelekwa katika uhamisho na kutupwa mbali; nani basi aliyewalea watoto hawa? Mimi niliachwa peke yangu, sasa, hawa wametoka wapi?


Ewe Yerusalema, uliteseka, ulitaabishwa na kukosa wa kukufariji, lakini nitakujenga upya kwa mawe ya bei kali, misingi yako itakuwa ya mawe ya yakuti.


Lakini hema yangu imebomolewa, kamba zake zote zimekatika; watoto wangu wameniacha, na kujiendea, wala hawako tena; hakuna wa kunisimikia tena hema yangu, wala wa kunitundikia mapazia yangu.


Agano hili halitakuwa kama lile nililofanya na babu zao nilipowatoa kwa mukono wangu kutoka Misri; agano hilo walilivunja, ingawa mimi nilikuwa Bwana wao.


Kweli, kondoo walisambazwa, wakatangatanga juu ya milima na vilima. Kondoo walisambazwa katika dunia yote, na hakukukuwa mutu aliyejali juu yao wala kuwatafuta.


Umeanguka na hautainuka tena ewe binti Israeli! Umeachwa ukiwa katika inchi yako, hakuna hata mutu wa kukuinua.


Muwaache! Wao ni vipofu, wanaongoza vipofu wengine. Na kama kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, wote wawili wanatumbukia ndani ya shimo.”


Yesu alipoona kundi la watu, aliwasikilia huruma, kwa maana walikuwa wamesumbuka na kuregea, kama kondoo wasiokuwa na muchungaji.


Yesu akashika mukono wa yule kipofu na kumupeleka inje ya kijiji. Yesu alipokwisha kupakaa mate kwa macho ya mutu yule na kuweka mikono juu yake, akamwuliza: “Unaona kitu?”


Basi, sasa Bwana atakuazibu, nawe utakuwa kipofu, wala hautaweza hata kidogo kuona mwangaza kwa muda.” Mara moja macho ya Elema yakaingiwa na giza hata yakapofuka, naye akaanza kupapasapapasa akitafuta mutu wa kumwongoza.


Saulo akasimama wima, na ingawa macho yake yalikuwa wazi hakuweza kuona kitu. Halafu wakamushika mukono na kumwongoza mpaka ndani ya muji Damasiki.


Agano lile halitakuwa sawa na lile nililofanya na babu zao siku nilipowakamatia kwenye mukono na kuwaondoa toka inchi ya Misri. Kwa sababu hawakushika lile agano, kwa hiyo vilevile sikuwashugulikia. Ni Bwana wetu Mungu anayesema hivyo.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις