Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Isaya 50:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Nilipokuja, kwa nini sikukuta mutu? Nilipoita mbona hamukuitikia? Mukono wangu ni mufupi hata nisiweze kuwaokoa ninyi? Sina nguvu ya kuwakomboa? Ninakausha bahari kwa kuikaripia, na mito ninaifanya kuwa jangwa; samaki wake wanakufa na kunuka kwa kukosa maji.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Isaya 50:2
46 Σταυροειδείς Αναφορές  

Kuna jambo lolote lisilowezekana kwa Yawe? Nitakurudilia wakati uliopangwa, kwa wakati kama huu katika mwaka, na Sara atakuwa na mutoto mwanaume.”


Musidanganywe na Hezekia wala musishawishiwe kwa hayo. Musimwamini mutu huyu, kwa maana hakujatokea mungu wa taifa au mufalme yeyote aliyeweza kuwakomboa watu wake kutoka mikono ya mufalme wa Asuria. Vile vile mungu wenu hataweza!”


Alikaripia bahari Nyekundu, ikakauka; akawapitisha humo kama katika inchi kavu.


Mungu aligeuza mito kuwa jangwa, chemichemi akazikausha kabisa.


Musa akanyoosha mukono wake juu ya bahari, naye Yawe akasukuma bahari nyuma kwa upepo mukali toka upande wa mashariki. Upepo ule ulivuma usiku kucha, ukagawanya bahari sehemu mbili na katikati kukatokea inchi kavu.


Lakini Waisraeli walipita katikati ya bahari pahali pakavu, kuta za maji zikiwa zimesimama upande wao wa kuume na wa kushoto.


Samaki wanaokuwa ndani ya muto Nili watakufa, muto wote utanuka vibaya, na Wamisri watachukia kabisa kunywa maji yake.’ ”


Samaki wakakufa, muto ukanuka vibaya sana hata Wamisri hawakuweza kunywa maji yake. Inchi nzima ikajaa damu.


“Nimewaita nanyi mumekataa kusikiliza, nimewanyooshea mukono mukuje nanyi hamukujali,


Yawe atakausha guba ya bahari ya Misri, kwa pumzi yake inayochoma atakausha muto Furati, nao utagawanyika katika vijito saba, watu wavuke humo miguu mikavu.


Maji ya muto Nili yatakaushwa, nao utakauka kabisa.


Yawe ameunyoosha mukono wake juu ya bahari amezitetemesha falme; ametoa amri kuharibu makimbilio ya Kanana.


Ni nani kati ya miungu ya inchi hizi aliyeokoa inchi zao toka katika mikono yangu. Yawe ataweza kuuokoa Yerusalema?”


Nimeangalia vizuri sana, lakini simwoni mutu yeyote; hakuna yeyote kati ya hao miungu anayeweza kushauri; nikiuliza, hakuna anayeweza kunijibu.


Nitaharibu milima na vilima, na majani yote nitayakausha. Mito ya maji nitaigeuza kuwa inchi kavu, na visima vya maji nitavikausha.


Zamani Yawe alifanya barabara katika bahari na kuweka njia kati ya maji mengi. Alipiga kundi la waaskari lenye nguvu, kundi la magari na farasi wa vita, waaskari na mashujaa wa vita. Aliwaangusha chini hata hawawezi kusimama tena, Aliwakomesha na kuwazimisha kama utambi wa taa. Sasa Yawe anasema hivi:


Mimi ndiye ninayeviamuru vilindi: Mukauke, nitakausha mito yenu.


Wewe ndiwe uliyekausha bahari, ndiwe uliyevikausha vilindi vya maji na kufanya njia katika vilindi vya bahari, kusudi wale uliowakomboa wavuke humo.


Yerusalema, Yawe amekuita tena. Ulikuwa kama vile muke aliyeachwa na kuhuzunika. Mungu wako anasema: Muke aliyeolewa akiwa kijana, anaweza kuachiliwa?


Musifikiri kwamba mukono wa Mungu ni mufupi, hata asiweze kuwaokoa, au kwamba masikio yake yamefungana, hata asiweze kuwasikiliza ninyi.


Aliona kwamba hakuna mutu aliyejali, akashangaa kwamba hakuna aliyeingilia kati. Basi akaamua kunyoosha mukono wake mwenyewe, haki yake ikamusaidia.


Aliwaongoza katikati ya vilindi vya bahari, wakapita humo kama farasi bila kujikwaa.


Hakuna hata mumoja anayekuja kukuomba; hakuna anayejishugulisha kukutafuta. Wewe unauficha uso wako mbali nasi, umetuacha tufungwe na maovu yetu.


Nimewapangia kifo kwa upanga, ninyi wote mutanaswa kwa kuchinjwa! Maana, nilipowaita, hamukuniitikia; niliposema, hamukunisikiliza. Mulitenda maovu mbele yangu, mukachagua yale nisiyoyapenda.


Basi, nitawaletea taabu; zile hasara zote wanazoogopa zitawapata; maana nilipoita hakuna aliyeitika, niliposema hawakunisikiliza. Lakini walifanya maovu mbele yangu, walichagua yale ambayo hayanipendezi.


Namna gani unakuwa kama mutu aliyechanganyikiwa, kama shujaa asiyeweza kusaidia mutu? Ingawa hivyo wewe ee Yawe unakaa katikati yetu; nasi tunajulikana kwa jina lako, usituache.


Ile amri ambayo Yonadabu mwana wa Rekabu aliwapa wana wake kwamba wasikunywe divai, imefuatwa; nao hawakunywi divai mpaka siku hii ya leo, maana wametii amri ya babu yao. Lakini mimi nilisema nanyi tena na tena, nanyi hamukunisikiliza.


Niliwapelekea tena na tena watumishi wangu wote, ni kusema manabii wawaambie kila mumoja wenu aachane na mwenendo wake mwovu, abadilishe matendo yake na kuacha kuifuata na kuitumikia miungu mingine. Na kwamba mukifanya hivyo mutakaa katika inchi niliyowapa ninyi na babu zenu. Lakini ninyi hamukunitegea sikio wala hamukunisikiliza.


Mukimbie huko na huko katika Yerusalema, mupeleleze na kujionea wenyewe, muchunguze katika masoko yake. Mukiona hata mutu mumoja anayefuata sheria, mutu anayetafuta ukweli, basi Yawe atausamehe Yerusalema.


Ninyi mumefanya mambo hayo yote. –Ni ujumbe wa Yawe.– Na hata niliposema nanyi tena na tena hamukunisikiliza. Nilipowaita hamukuitika.


Sasa wewe Yeremia utawaambia maneno haya yote, lakini wao hawatakusikiliza. Utawaita, lakini hawatakuitikia.


Mimi nilisikiliza kwa uangalifu, lakini wao hawakusema ukweli wowote. Hakuna mutu anayetubu uovu wake, wala kujiuliza hivi: Nimefanya nini? Kila mumoja wao anashika njia yake, kama farasi anavyokimbia haraka kwa vita.


Basi, mutakaposikia tena sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na sauti za ala nyingine za muziki, muko tayari kuinama chini na kuiabudu sanamu niliyotengeneza? Kama mukikataa, mutatupwa mara moja katika furu la moto mukali. Ni mungu gani anayeweza kuwaokoa katika mikono yangu?


Kwa hiyo, ninaamuru kwamba watu wa kabila lolote, taifa lolote au luga yoyote, watakaosema kitu chochote cha kumuzarau Mungu wa Sadiraki, Mesaki na Abedenego, watakatwa vipandevipande na nyumba zao zitabomolewa. Maana hakuna mungu mwingine anayeweza kuokoa namna hii.


Ilipokuwa asubui mapema, mufalme Dario aliamuka, akaenda kwa haraka kwenye pango la simba.


Ninatoa amri katika ufalme wangu kwamba watu wote wanapaswa kumwogopa na kumuheshimu Mungu wa Danieli. Yeye ni Mungu Mwenye Uzima, anayeishi milele; ufalme wake hauwezi kuangamizwa hata kidogo, utawala wake hauna mwisho.


Lakini kadiri nilivyozidi kuwaita, ndivyo walivyozidi kwenda mbali nami; waliendelea kuyatambikia Mabali, na kuvifukizia ubani sanamu za miungu.


Watu wangu wamekusudia kuniacha mimi, wakiitwa kusimama wapande juu, hakuna hata mumoja anayeweza.


Anaikaripia bahari na kuikausha, yeye anaikausha mito yote. Mbuga za Basani na mulima Karmeli zinanyauka, maua ya Lebanoni yanakauka.


Ee Yawe, umeikasirikia mito? Umeyakasirikia maji ya bahari? Ulipanda juu ya gari lako la vita na kuendesha farasi kwa kupata ushindi.


Yawe akamujibu Musa: Uwezo wangu umepunguka? Utaona basi kama neno langu litakuwa la kweli kwako au hapana.


Yesu akaamuka, akakaripia ile zoruba na kuiambia ziwa: “Kimya! Tulizana!” Basi zoruba ikakoma na kukakuwa kimya kabisa.


Alikuja katika inchi yake, lakini taifa lake halikumupokea.


Hukumu inatokana na hivi: mwangaza umekuja katika ulimwengu, lakini watu wanapenda giza kuliko mwangaza, kwa sababu matendo yao ni mabaya.


maji yaliyokuwa yanatiririka kutoka upande wa juu yalisimama na kulundikana mpaka kule Adamu kijiji kinachokuwa karibu na muji wa Zaretani. Maji yaliyokuwa yanateremuka kwenda katika bahari ya Araba, ni kusema bahari ya Chumvi, yalitoweka kabisa, watu wakavuka mbele ya Yeriko.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις