Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Isaya 48:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Wewe uliyasikia na sasa unayaona yote. Kwa nini hauwezi kuyakubali? Tangu sasa nitakujulisha mambo mapya; mambo yaliyofichwa ambayo haukuyajua.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Isaya 48:6
29 Σταυροειδείς Αναφορές  

Wenye hekima wafikiri juu ya mambo haya, watambue wema wa Yawe.


Nitarudiliarudilia kwa sauti maamuzi yako yote uliyotoa.


Ewe Israeli, watu wangu, enyi muliotwangwa na kupepetwa kama ngano. Sasa nimewaambia ninyi mambo niliyoyasikia kwa Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli.


Ninyi mumeona mambo mengi, lakini hamuelewi kitu. Masikio yenu yako wazi, lakini hamusikii kitu!


Jina langu mimi ni Yawe; sitamupa mwingine utukufu wangu, wala sifa zangu sanamu za miungu.


Mambo niliyotabiri yametukia; na sasa ninatangaza mambo mapya, ninakuelezea hayo mbele hayajatukia.


Muangalie, mimi ninafanya kitu kipya. Kinafanyika sasa hivi, nanyi mutaweza kukiona. Nitafanya njia katika mbuga, na kububujisha mito katika jangwa.


Mambo hayo yanatukia sasa; haukupata kuyasikia mbele ya siku ya leo, hivyo hauwezi kusema: Aa! Nilikwisha kuyajua.


Enyi watu! Musikilize vile mimi Yawe ninavyosema: Nimekuwa kama vile jangwa au inchi yenye giza kubwa? Kwa nini basi watu wangu wanasema: Sisi tuko watu huru; hatutakurudilia!


Uniite, nami nitakujibu na kukuambia mambo makubwa yaliyofichwa ambayo haujapata kuyajua.


Mutangaze kati ya mataifa, munyanyue bendera na kutangaza, musifiche jambo lolote. Museme: Babeli umetekwa, mungu Beli amepatishwa haya. Merodaki amefazaishwa; sanamu zake zimefezeheshwa, miungu yake imefazaishwa.


Baragumu ya vita inalia katika muji bila kutia watu hofu? Muji unaweza kupatwa na hasara ambayo haikuletwa na Mungu?


Yawe anawaita wakaaji wa muji, na ni jambo la hekima sana kumutii yeye: Musikilize, enyi watu wa Yuda; musikilize enyi muliokusanyika katika muji.


Neno ninalowaambia katika giza, muliseme muchana kati. Vilevile neno munalosikia kwa siri, mulitangaze mukisimama juu ya paa ya nyumba.


Siwaiti ninyi tena watumishi, kwa sababu mutumishi hajui mambo bwana wake anayofanya. Ninawaita ninyi warafiki kwa sababu nimewajulisha yote niliyosikia kutoka kwa Baba yangu.


Lakini mutapokea uwezo wakati Roho Mutakatifu atakaposhuka juu yenu. Nanyi mutakuwa washuhuda wangu katika Yerusalema, katika Yudea yote na Samaria na hata katika inchi zote za dunia.”


Lakini ni kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Mambo yale ambayo hakuna mutu aliyepata kuyaona wala kuyasikia, mambo yale ambayo hakuna mutu aliyepata kufikiri juu yake, ndiyo yale Mungu aliyowatayarishia wale wanaomupenda.”


Basi uandike mambo unayoona, na mambo yanayokuwa sasa na yale yatakayotokea nyuma.


Nyuma ya mambo hayo nilipata maono mengine. Niliona mulango mumoja umefunguliwa wazi mbinguni. Halafu ile sauti niliyosikia mara ya kwanza, iliyolia kama baragumu, ikaniambia: “Panda huku, nami nitakuonyesha mambo yanayopaswa kutokea nyuma ya hayo ya mbele.”


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις