Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Isaya 47:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Mukombozi wetu ndiye Mutakatifu wa Israeli; Yawe wa majeshi ndilo jina lake.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Isaya 47:4
12 Σταυροειδείς Αναφορές  

Unikinge mimi mutumishi wako na makosa ya makusudi, usikubali hayo yanitawale. Hapo nitakuwa mukamilifu, wala sitakuwa na kosa kubwa.


Enyi watu wa Yakobo zaifu kama mududu, enyi Waisraeli, musiogope! Nitawasaidia. –Ni ujumbe wa Yawe.– Mukombozi wenu ni yule Mutakatifu wa Israeli.


Yawe, Mukombozi wenu, Mutakatifu wa Israeli, anasema hivi: Kwa ajili yenu nitatuma waaskari kwenda Babeli. Nitavunja vifungio vya milango ya muji wake, na kelele za wale Wakaldea zitageuka maombolezo.


Mimi ni Yawe, Mutakatifu wenu; Mimi ndiye Muumba wa Israeli, Mufalme wenu.


Maana mimi ni Yawe, Mungu wenu, Mungu Mutakatifu wa Israeli, Mwokozi wenu. Ninaitoa inchi ya Misri kwa ajili ya ukombozi wenu, ninaitoa Kushi na Seba kusudi muachwe huru.


Yawe, Mufalme na Mukombozi wa Israeli, Yawe wa majeshi anasema hivi: Mimi ni wa kwanza na wa mwisho; hakuna mungu mwingine isipokuwa mimi.


Nitawasukuma watesaji wako wakule miili yao wenyewe; watalewa damu yao wenyewe kama divai. Halafu wanadamu wote watatambua kwamba mimi ni Yawe, Mwokozi wako, Mukombozi wako, Mwenye Nguvu wa Yakobo.


Mimi ni Yawe, Mungu wako, ninayechafua bahari, zoruba yake ikinguruma; Yawe wa majeshi, ndilo jina langu!


Muumba wako atakuwa mume wako. Jina lake Yawe wa majeshi. Mukombozi wako ni Mutakatifu wa Israeli. Yeye anaitwa Mungu wa Ulimwengu Wote.


Maana mimi Yawe nimemukomboa Yakobo, nimemwokoa kutoka kwa wenye nguvu kuliko yeye.


Mungu ndiye aliyeifanya milima, na kuumba upepo; ndiye anayemujulisha mwanadamu mawazo yake; ndiye anayegeuza muchana kuwa usiku, na kukanyaga vilele vya dunia. Yawe wa majeshi ndilo jina lake!


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις