Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Isaya 47:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Watu watauona uchi wako; wataona haya yako. Mimi nitalipiza kisasi, wala sitamuhurumia mutu yeyote.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Isaya 47:3
27 Σταυροειδείς Αναφορές  

Mara moja macho yao yakafumbuliwa, wakatambua kwamba wako uchi. Kwa hiyo wakashona majani ya muti wa tini, wakajifanyia nguo.


Basi, mufalme wa Asuria atawapeleka Wamisri na Wakushi kuwa wafungwa, wakubwa kama vile wadogo. Watapelekwa, nao watatembea uchi na bila viatu, matako wazi. Misri ipate haya!


Basi, mimi Yawe nitawaazibu; nitawanyoa nywele hao wanawake wa Sayuni, na kuwavua nguo za kufunika uchi wao.


Muwaambie waliovunjika moyo: Mujipe moyo, musiogope! Muangalie Mungu wenu atakuja kulipiza kisasi, atakuja kuwaazibu waadui zenu; atakuja yeye mwenyewe kuwaokoa ninyi.


Nawe utajiuliza hivi katika moyo wako: Kwa nini mambo haya yamenipata? Sawa! Ikiwa kanzu yako imepandishwa, na kutendewa kwa kinguvu, hayo ni matokeo ya makosa yako mengi sana.


Nitapandisha kanzu yako mpaka kwenye kichwa hata uchi wako upate kuonekana wazi.


Yawe amezichochea roho za wafalme wa Wamedi, kwa maana amekusudia kuiangamiza Babeli. Kweli, hicho ndicho kisasi cha Yawe; analipiza kisasi kwa ajili ya hekalu lake. Munoe mishale yenu! Mutwae ngao!


Wataanguka na kuuawa katika inchi ya Wakaldea, wataumizwa katika barabara zake.


Kweli, mwangamizaji anashambulia Babeli; waaskari wake wametekwa, pinde zao zimevunjwavunjwa. Mimi Yawe ni Mungu mwenye kuazibu, hakika mimi nitalipiza kisasi kamili.


Basi, mimi nitawakusanya wapenzi wako wote uliojifurahisha nao, wote uliowapenda na wote uliowachukia. Nitawakusanya toka pande zote wakushambulie. Nitawafunulia uchi wako wapate kuuona.


Mimi Yawe wa majeshi ninasema nitakushambulia; nitapandisha nguo yako mpaka kwenye kichwa, niyaache mataifa yauone uchi wako, falme zitaona haya yako.


Wandugu wapendwa, musilipize kisasi ninyi kwa ninyi, lakini mumwachie Mungu wakati wa kutenda kufuatana na kasirani, maana imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Ni kazi yangu kulipiza kisasi. Ni mimi nitakayelipiza.”


Ni kazi yangu kulipiza kisasi, mimi nitalipiza, wakati miguu yao itakapoteleza; maana siku yao ya hasara imefika mwisho wao uko karibu sana.


Na ule muji mukubwa ukagawanyika katika sehemu tatu, na miji ya mataifa yote ikabomoka. Mungu hakusahau muji mukubwa Babeli, akaukunywesha kikombe kinachokuwa na divai ya kasirani yake kali.


Enyi mbingu, nanyi watu wa Mungu pamoja na mitume na manabii wake, mufurahi kwa ajili ya mambo yaliyotokea muji ule, kwa maana Mungu amewapatia haki yenu kwa kuuhukumu!


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις