Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Isaya 45:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Ole kwake mutu anayebishana na Muumba wake: chombo cha udongo kubishana na mufinyanzi wake! Udongo unamwuliza anayeufinyanga: Unatengeneza nini hapa? au kumwambia: Kazi yako si kamili!

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Isaya 45:9
22 Σταυροειδείς Αναφορές  

Kumbuka kwamba uliniumba kwa udongo. Utanirudisha tena katika mavumbi?


Kwa nini unashindana naye, ukisema hatajibu ulizo lako moja?


Wewe mwenye kuchunguza makosa utashindana na Mungu Mwenye Uwezo? Wewe unayebishana nami Mungu, basi ujibu mambo hayo!


Yeye akitwaa kitu kwa rafla, nani anayeweza kumuzuia? Nani anayeweza kumwuliza: “Unafanya nini?”


Yeye ni mwenye hekima sana na nguvu nyingi. Nani aliyepingana naye, akashinda?


Hakuna hekima, ufahamu, wala shauri yoyote ya mutu, itakayoweza kupingana na Yawe.


Kila kitu kinachotukia kilikwisha kupangwa tangu zamani. Hali ya mwanadamu inajulikana, na tunajua kwamba muzaifu hawezi kubishana na mutu mwenye nguvu zaidi.


Shoka litaweza kujisifu mbele ya yule anayelitumia? Musumeno unaweza kujivuna mbele ya mwenye kukata nao? Ni kama kwamba vile fimbo ingeweza kumwinua anayeishika, au gongo kumwinua mwenye kuitumia!


Ninyi munafanya mambo kinyume kabisa! Mufinyanzi na udongo ni hali moja? Chombo hakiwezi kumwambia aliyekitengeneza hivi: Wewe haukunitengeneza. Kilichofinyangwa hakiwezi kumwambia aliyekiumba; Wewe haujui kitu.


Ole kwake mutu anayemwambia baba: Umezaa nini? au anayemwambia mama: Umeleta nini katika dunia?


Hata hivyo, ee Yawe, wewe ni Baba yetu. Sisi ni kama udongo, wewe ni mufinyanzi. Sisi wote ni kazi ya mikono yako.


Usitukasirikie sana, ee Yawe, usiukumbuke uovu wetu siku zote! Ukumbuke kwamba sisi wote ni watu wako!


Enyi Waisraeli! Mimi siwezi kuwafanya ninyi kama mufinyanzi huyu anavyofanya? –Ni ujumbe wa Yawe.– Mujue kwamba kama vile udongo unavyokuwa katika mikono ya mufinyanzi, ndivyo ninyi munavyokuwa katika mikono yangu.


Nawe utamwambia huyo Yoyakimu mufalme wa Yuda kwamba: Yawe anasema hivi: Umekichoma kwa moto kitabu hicho na kuuliza kwa nini Yeremia ameandika kwamba mufalme wa Babeli atakuja kuiharibu inchi hii na kuwaangamiza watu na nyama!


Ewe Babeli, nilikutegea mutego ukanaswa, wala haukujua kitu juu yake; ulipatikana, ukakamatwa, kwa sababu ulishindana nami Yawe.


Au tunataka kumuchokoza Bwana hata asikie wivu? Munafikiri kuwa sisi tuko na nguvu kuliko yeye?


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις