Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Isaya 43:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Maana mimi ni Yawe, Mungu wenu, Mungu Mutakatifu wa Israeli, Mwokozi wenu. Ninaitoa inchi ya Misri kwa ajili ya ukombozi wenu, ninaitoa Kushi na Seba kusudi muachwe huru.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Isaya 43:3
29 Σταυροειδείς Αναφορές  

Wana wa Kushi walikuwa Seba, Havila, Sabuta, Rama na Sabuteka. Wana wa Rama walikuwa Seba na Dedani.


Wafalme wa Tarsisi na visiwa wamulipe kodi, wafalme wa Sheba na Seba wamuletee zawadi.


Viongozi wa mufalme wakamwuliza: “Mutu huyu atatusumbua mpaka wakati gani? Uwaache watu hawa wajiendee wamutumikie Yawe, Mungu wao. Haujali kwamba inchi ya Misri inaangamia?”


Mimi ni Yawe, Mungu wako, niliyekutoa katika inchi ya Misri, ambako ulikuwa mutumwa.


Mutu wa haki anaokolewa katika shida, na mwovu anaingia mule kwa pahali pake.


Mwovu atakuwa malipo kwa ukombozi wa wenye haki; nao wasiokuwa waaminifu kwa pahali pa watu wa usawa.


Mazabahu hayo yatakuwa kitambulisho na ushuhuda kwa Yawe wa majeshi katika inchi ya Misri. Watu wakimulilia Yawe humo kwa sababu ya kugandamizwa, yeye atawapelekea mukombozi atakayewatetea na kuwakomboa.


Yawe akasema: Mutumishi wangu Isaya amekuwa akitembea uchi na bila viatu kwa muda wa miaka mitatu sasa, kama kitambulisho juu ya inchi za Misri na Kushi.


Mugeuke na kuiacha njia ya ukweli; musituambie tena juu ya Mungu, Mutakatifu wa Israeli.


Enyi watu wa Yakobo zaifu kama mududu, enyi Waisraeli, musiogope! Nitawasaidia. –Ni ujumbe wa Yawe.– Mukombozi wenu ni yule Mutakatifu wa Israeli.


Jina langu mimi ni Yawe; sitamupa mwingine utukufu wangu, wala sifa zangu sanamu za miungu.


Mimi peke yangu ndiye Yawe, hakuna mukombozi mwingine isipokuwa mimi.


Yawe anasema hivi: Utajiri wa Misri na faida ya uchuuzi za Kushi, pamoja na za watu wa Seba, wale watu warefu sana, zitakuja kwako mwenyewe wewe taifa la Israeli, zote zitakuwa mali yako. Watu hao watakufuata wakifungwa minyororo; watainama mbele yako na kukusihi wakisema: Kwako kuna Mungu wa kweli, wala hakuna Mungu mwingine lakini yeye.


Kweli wewe ni Mungu mwenye kufichama, Mungu wa Israeli, Mungu mwokozi.


Mutangaze na kusema habari zenu. Mufanye shauri pamoja! Ni nani aliyetangaza zamani matukio ya sasa? Ni nani aliyesema mambo haya zamani? Haikukuwa mimi Yawe? Hakuna Mungu mwingine isipokuwa mimi! Mimi ni Mungu wa haki na mwokozi; hakuna mwingine isipokuwa mimi.


Nitawasukuma watesaji wako wakule miili yao wenyewe; watalewa damu yao wenyewe kama divai. Halafu wanadamu wote watatambua kwamba mimi ni Yawe, Mwokozi wako, Mukombozi wako, Mwenye Nguvu wa Yakobo.


Utaletewa chakula na watu wa mataifa; wafalme watakupatia chakula bora. Hapo utatambua kwamba mimi Yawe ni Mwokozi wako; mimi Mwenye Nguvu wa Yakobo ni Mukombozi wako.


Maana alisema juu yao: Hakika, hawa ni watu wangu; watoto wangu ambao hawatanidanganya. Basi yeye akakuwa Mwokozi wao.


Wewe unayekuwa tumaini la Waisraeli, wewe unayetuokoa wakati wa taabu, namna gani unajifanya kama mugeni katika inchi, kama musafiri anayelala kwa usiku mumoja tu?


Kwa hiyo, Yawe anasema: Wakati huu nitawafundisha kusudi wapate kutambua waziwazi nguvu zangu na uwezo wangu, nao watajua kwamba jina langu ni Yawe.


Nitajulisha jina langu takatifu kwa watu wangu Waisraeli, wala sitaruhusu tena watu walikufuru jina langu takatifu. Nayo mataifa yatatambua kwamba mimi ni Yawe, Mutakatifu wa Israeli.


Yawe anasema: Lakini mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika inchi ya Misri; hakuna mungu mwingine lakini mimi, wala hakuna anayeweza kuwaokoa.


Kwa sababu mimi ni Yawe, Mungu wenu, mujitakase na kuwa watakatifu kwa maana mimi ni mutakatifu. Wala musijichafue na kitu chochote kinachotambaa juu ya inchi.


Kwangu mimi, ninyi Waisraeli, muko sawasawa na watu wa Kushi! –Ni ujumbe wa Yawe.– Niliwatoa Wafilistini kutoka Krete, na Waaramu kutoka Kiri, kama nilivyowatoa ninyi kutoka Misri.


Mushangilie sana enyi watu wa Sayuni! Mupige vigelegele, enyi watu wa Yerusalema! Angalia, mufalme wenu anawakujia, anakuja kwa shangwe na ushindi! Ni mupole, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, mutoto wa punda.


yeye anayekuwa Mungu peke yake, Mwokozi wetu, asifiwe na kuwa na ukubwa, uwezo na mamlaka, kwa njia ya Yesu Kristo Bwana wetu, tangia zamani za kale, sasa na hata milele! Amina.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις