Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Isaya 40:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Mutamulinganisha Mungu na nini basi, au ni kitu gani cha kumufananisha nacho?

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Isaya 40:18
24 Σταυροειδείς Αναφορές  

Una nguvu kama mimi Mungu? Unaweza kunguruma kwa sauti kama yangu?


Nani anayekuwa kama Yawe, Mungu wetu? Yeye anakaa juu kabisa;


Ee Yawe, mbingu zinasifia maajabu yako, uaminifu wako unasifiwa katika kusanyiko la watakatifu.


Nani katika mbingu anayeweza kulinganishwa nawe, ee Yawe? Nani anayekuwa sawa nawe kati ya miungu?


Wewe unatisha katika baraza la watakatifu; wote wanaokusanyika mbele yako wanakuheshimu na kukuogopa.


“Ewe Yawe, ni nani kati ya miungu anayelingana nawe? Ni nani aliyekuwa kama wewe unayekuwa mutakatifu mukubwa, unayetisha kwa matendo matukufu, unayetenda mambo ya ajabu?


Usijifanyie sanamu ya miungu, wala mufano wa kitu chochote kinachokuwa juu mbinguni, wala kinachokuwa chini katika dunia, wala kinachokuwa ndani ya maji chini ya dunia.


Watu wakawakusanya vyura wale malundomalundo. Inchi nzima ikanuka.


Maana mara hii, wewe mwenyewe, wakubwa wako na watu wako mutapatwa na mapigo yangu makali. Nawe utatambua kwamba hakuna yeyote katika dunia anayekuwa kama mimi.


Mungu Mutakatifu anauliza hivi: Basi, mutanilinganisha na nani? Kuna mutu anayeweza kuwa sawasawa mimi?


Yawe, Mufalme na Mukombozi wa Israeli, Yawe wa majeshi anasema hivi: Mimi ni wa kwanza na wa mwisho; hakuna mungu mwingine isipokuwa mimi.


Mutanifananisha na nani na kunisawanisha naye? Mutanilinganisha na nani nipate kuwa sawasawa naye?


Mukumbuke mambo niliyotenda hapo zamani! Mimi ni Mungu. Hakuna Mungu mwingine. Mimi ni Mungu. Hakuna mwingine kama mimi.


Enyi Waisraeli musikilize neno Yawe analowaambia.


Lakini Mungu wa Yakobo si kama sanamu hizo, maana, yeye ndiye aliyeumba vitu vyote, na Israeli ni taifa linalokuwa mali yake; Yawe wa majeshi, ndilo jina lake.


Ee Yawe, hakuna anayekuwa kama wewe; wewe ni mukubwa na nguvu yako inajulikana.


Ee Mungu, ni nani anayekuwa kama wewe? Wewe unasemehe zambi za watu wako waliobaki, wala hauyaangalii makosa yao. Hasira yako haidumu milele, lakini unapendelea zaidi kutuonyesha wema wako.


Basi kwa kuwa sisi tuko watoto wa Mungu, tusiwaze kwamba anafanana na sanamu ya zahabu au ya feza au ya jiwe, iliyochorwa kwa ufundi na akili ya watu.


Musa akamalizia kwa kusema: “Ee Israeli, hakuna anayekuwa kama Mungu wako, yeye anayeruka toka mbinguni kuja kukusaidia, anapita juu katika anga katika utukufu wake.


“Kwa hiyo mukuwe waangalifu kusudi musisahau kwamba Yawe aliposema nanyi kule kwenye milima ya Horebu katikati ya moto hamukumwona kwa umbo. Kwa sababu hiyo mufanye angalisho sana,


Kristo ni mufano kamili wa Mungu asiyeonekana. Yeye ni muzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.


Yeye ni kitambulisho cha mwangaza wa utukufu wa Mungu, kwa maana yeye ni mufano kamili pahali ya Mungu mwenyewe, na kwa uwezo wa neno lake analinda vitu vyote. Naye alipokwisha kuwatakasa watu toka katika zambi zao, aliikaa na mamlaka katika mbingu kwa kuume kwa Mungu Mwenye Uwezo wote.


Hakuna anayekuwa mutakatifu kama Yawe; hakuna yeyote anayekuwa kama yeye; hakuna anayekuwa jiwe la kufichamia kama Mungu wetu.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις