Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Isaya 40:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Atachunga kundi lake kama muchungaji, atawakusanya wana-kondoo katika mikono yake, atawabeba kwa kifua chake, na atawaongoza polepole kondoo wanaonyonyesha.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Isaya 40:11
32 Σταυροειδείς Αναφορές  

Lakini Yakobo akamwambia: “Bwana wangu, wewe unajua kwamba watoto hawa ni wachanga, na kwamba nyama hawa wananyonyesha, nami ninapaswa kuwatunza. Kama nyama hawa watapelekwa mbio kwa siku moja, wote watakufa.


Lakini upinde wake bado imara, na mikono yake imepewa nguvu, kwa uwezo wa Mwenye Nguvu wa Yakobo, kwa jina la Muchungaji, Mulinzi wa Israeli.


Mujue kwamba Yawe ndiye Mungu. Yeye ndiye aliyetuumba, sisi ni mali yake; sisi ni watu wake na kondoo wake anaowachunga.


Hata kama wazazi wangu wakinitupa, Yawe atanipokea kwake.


Ee Mungu, uwaokoe watu wako; uwabariki watu hao wanaokuwa mali yako. Ukuwe muchungaji wao na kuwalinda milele.


Umutumainie Yawe na kutenda mazuri, upate kuishi katika inchi na kuwa salama.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo. Zaburi ya Asafu.


Hatavunja tete lililokunjama, hatazimisha utambi unaotoa moshi; ataimarisha sheria yangu kwa uaminifu.


Halafu walikumbuka siku za zamani, wakati wa Musa, mutumishi wa Yawe. Wakauliza: Yuko wapi sasa Yawe, aliyewaokoa wachungaji wa kundi lake katika bahari? Yuko wapi yule aliyeweka Roho wake Mutakatifu kati yao,


Enyi mataifa, musikilize neno langu mimi Yawe, mulitangaze katika visanga vya mbali, museme hivi: Aliyemusambaza Israeli, atamukusanya, atamutunza kama muchungaji anavyotunza kondoo wake.


Nitawarudisha kutoka inchi ya kaskazini, nitawakusanya kutoka miisho ya dunia. Wote watakuwa pale; hata vipofu na vilema, wanawake wenye mimba na wanaosikia maumivu ya kuzaa; kundi kubwa sana la watu litarudi hapa.


Mimi mwenyewe nitakuwa muchungaji wa kondoo wangu. Mimi mwenyewe nitawapumzisha. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Nitawatafuta kondoo waliopotea na waliotangatanga nitawarudisha kwa nyumba. Waliovunjika nitawatunza, na wale wanaokuwa zaifu nitawapatia nguvu. Lakini kondoo wanono na wenye nguvu nitawaangamiza. Mimi nitawachunga kondoo kama inavyostahili.


Wewe mwanadamu! Toa unabii juu ya wachungaji wa inchi ya Israeli. Uwaambie hao wachungaji kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ole kwenu ninyi wachungaji wa inchi ya Israeli, munaojikulisha ninyi wenyewe tu! Haiwapasi wachungaji kuwakulisha kondoo?


Nitaweka muchungaji mumoja juu yao, mufalme kama mutumishi wangu Daudi. Yeye atawakulisha na kuwa muchungaji wao.


Nanyi, ee kondoo wangu, ninyi ni watu wangu, nami ni Mungu wenu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Mutumishi wangu Daudi atakuwa mufalme wao; watakuwa na muchungaji mumoja tu. Watayafuata maagizo yangu na kushika masharti yangu.


Yeye ndiye atakayeleta amani. Waasuria wakishambulia inchi yetu, na kuingia katika nyumba zetu nzuri, tutatuma walinzi wetu wapigane nao, tutawapeleka waongozi wetu kwa wingi.


Ee Mungu, uwachunge watu wako kwa fimbo yako, uwachunge wale wanaokuwa kundi lako mwenyewe ambao wanaishi peke yao katika pori na kuzungukwa na inchi yenye mboleo. Uwachunge kama ulivyofanya pale zamani katika shamba la malisho ya Basani na Gileadi.


Basi, nikakuwa muchungaji wa kondoo ambao wachuuzi waliwatayarisha kwenda kuchinjwa. Nikatwaa fimbo mbili: moja nikaiita “Rehema”, na ingine nikaiita “Umoja”, nikaenda kuchunga kondoo.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Amuka, ee upanga! Simama umushambulie muchungaji wangu, muchungaji anayenitumikia. Umuue muchungaji na kondoo watawanyike. Nitaunyoosha mukono wangu kwa kuwashambulia watu wazaifu.


Mungu wa amani, aliyemufufua Bwana wetu Yesu ambaye ni Muchungaji mukubwa wa kondoo kwa njia ya kumwanga damu yake inayohakikisha agano la milele,


Kwa maana mulikuwa kama kondoo wanaopotea, lakini sasa mumerudi kwa yule anayekuwa muchungaji na mwangalizi wa roho zenu.


Na wakati Muchungaji Mukubwa atakapotokea, mutapokea taji ya utukufu isiyoweza kuharibika.


Kwa maana Mwana-Kondoo anayekuwa katikati ya kiti cha kifalme, atawachunga na kuwaongoza kwenye chemichemi ya maji ya uzima. Naye Mungu atawapanguza machozi yao yote.”


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις