10 Nilisema: nikiwa mubichi kabisa, inanipasa niage dunia. Mimi nimepangiwa kwenda katika kuzimu siku zote zilizonibakilia.
Sina nguvu ya kuweza kuendelea. Sijui mwisho wangu utakuwa namna gani, nipate kuvumilia.
Kumbuka, maisha yangu ni pumzi tu; jicho langu halitaona jambo zuri lolote tena.
Mungu amenipunguzia nguvu ningali kijana; amefupisha maisha yangu.
Ee Mungu wangu, usinihamishe sasa wakati ningali bado kijana. Ee Yawe, wewe unadumu milele.
walichukizwa na chakula, walikuwa karibu kufa.
Nami niliogopa na kuzani kwamba ulikuwa umenitupa; kumbe, ulisikia kilio changu nilipokuita unisaidie.
Kila kitu unachotaka kufanya ukifanye kwa nguvu zako zote, maana, hakuna kazi, wala wazo, wala maarifa, wala hekima kule katika kuzimu unakokwenda.
Wakati ule, Hezekia aligonjwa sana karibu kufa. Halafu nabii Isaya mwana wa Amozi akamwendea, akamwambia: Yawe anasema hivi: Panga mambo yako sawasawa katika nyumba yako kwa sababu utakufa, hautapona.
Kisha mufalme Hezekia alipopona, akatunga wimbo huu wa shukrani:
Maji yalinizunguka na kunisonga; kilindi kilinifikia kila upande, majani ya bahari yakanifunika kichwa.
Tulikuwa tumefikiri kwamba tulihukumiwa kufa. Basi, ilitokea hivi kusudi tusijitegemee sisi wenyewe, lakini tumutegemee Mungu tu anayefufua wafu.