Hivi, Waisraeli wote walihesabiwa kufuatana na vizazi vyao na kuandikwa katika Kitabu cha Wafalme wa Israeli. Watu wa Yuda wamepelekwa katika utumwa mpaka Babeli kwa sababu ya kutokuwa waaminifu.
Sasa uwaulize wale watu waasi kama wanaelewa maana ya mufano huo. Uwaambie kwamba, mufalme wa Babeli alikuja Yerusalema, akamwondoa mufalme na wakubwa wake, akawapeleka Babeli.
Kisha akachagua mutu mumoja wa jamaa ya kifalme, akafanya naye mapatano, akamwapisha kiapo cha uaminifu. Aliwaondoa wakubwa wengine katika inchi akawapeleka mbali
Kisha Mungu akaniambia: Wewe mwanadamu, umeona mambo wazee wa Waisraeli wanayotenda kwa uficho, kila mutu katika chumba chake cha sanamu. Wanasema: Yawe hatuoni. Yawe ameiacha inchi.