Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Isaya 20:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Sargoni, mufalme wa Asuria, alimutuma jemadari wake mukubwa kushambulia muji wa Asidodi. Naye akaushambulia na kuuteka.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Isaya 20:1
9 Σταυροειδείς Αναφορές  

Kisha mufalme wa Asuria alimutuma majemadari wakubwa watatu pamoja na kundi kubwa la waaskari kutoka Lakisi kwenda kwa mufalme Hezekia kule Yerusalema. Walisafiri na kufika Yerusalema. Nao walipofika waliingia na kusimama karibu na mufereji wa kisima kinachokuwa upande wa juu katika barabara kubwa inayoelekea kiwanja cha mufuaji wa nguo.


Uzia akaondoka kwa kupigana vita na Wafilistini, akabomoa kuta za miji ya Gati, Yabune na Asidodi. Akajenga miji katika eneo la Asidodi na fasi ingine katika inchi ya Filistia.


Ulie ewe mulango; ulalamike ewe muji; tetemeka kwa hofu, ewe inchi yote ya Filistia. Maana moshi wa waaskari unakuja kutoka kaskazini, wala hakuna atakayechelewa katika makundi yake.


wageni wote walioishi katika inchi ya Misri; wafalme wote wa inchi ya Uzi; wafalme wote wa miji ya Wafilistini, Askeloni, Gaza, Ekuroni na mabaki ya Asidodi;


Nitaondoa wakaaji wa muji wa Asidodi, pamoja na mutawala wa Asikeloni. Nitanyoosha mukono wangu kwa kuazibu muji wa Ekuroni, na Wafilistini wote waliobaki wataangamia. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Hakuna mutu wa kabila la Anaki ambaye alibakia katika inchi ya Israeli; walibaki wachache tu katika miji ya Gaza, Gati na Asidodi.


Nyuma ya Wafilistini kuliteka Sanduku la Mungu, walilibeba kutoka muji wa Ebeni-Ezeri mpaka katika muji wao wa Asidodi.


Wafilistini walizipeleka zile sanamu tano za zahabu na za majipu kwa Yawe zikiwa sadaka ya malipo ya makosa yao, sanamu moja kwa ajili ya muji mumoja, muji wa Asidodi, muji wa Gaza, muji wa Asikeloni, muji wa Gati na kwa muji wa Ekuroni.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις