Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Isaya 19:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Nitawatia Wamisri katika mikono ya bwana mukali, mufalme mukali ambaye atawatawala. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Isaya 19:4
9 Σταυροειδείς Αναφορές  

Nitashangilia na kufurahia wema wako, maana wewe unaona taabu yangu, unajua huzuni yangu.


Mimi nitawachonganisha Wamisri wao kwa wao. Ndugu atapigana na ndugu yake, jirani atapigana na jirani yake, muji mumoja na muji mwingine, mufalme mumoja na mufalme mwingine.


Yawe akasema: Mutumishi wangu Isaya amekuwa akitembea uchi na bila viatu kwa muda wa miaka mitatu sasa, kama kitambulisho juu ya inchi za Misri na Kushi.


Basi, mufalme wa Asuria atawapeleka Wamisri na Wakushi kuwa wafungwa, wakubwa kama vile wadogo. Watapelekwa, nao watatembea uchi na bila viatu, matako wazi. Misri ipate haya!


Nitawatia katika mikono ya wale wanaotaka kuyaangamiza maisha yao, ni kusema Nebukadneza mufalme wa Babeli na wakubwa wake. Kisha, inchi ya Misri itakaliwa na watu kama ilivyokuwa hapo zamani. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitamupa Nebukadneza mufalme wa Babeli, inchi ya Misri. Atanyanganya mali yake yote, na kutwaa utajiri wa Misri kuwa mushahara wa waaskari wake.


Nitaukausha muto Nili na vijito vyake, na kuuzisha inchi ya Misri katika mikono ya watu waovu. Nitasababisha uharibifu katika inchi yote kwa mukono wa watu wageni. Ni Mimi Yawe ninayesema hivyo.


Hata hivyo, ulikamatwa mateka, watu wake wakapelekwa katika uhamisho. Hata watoto wake walipondwapondwa katika maingilio ya kila barabara; watu wake wenye heshima waligawanywa kwa kuwapigia kura, wakubwa wake wote walifungwa minyororo.


Saulo alipoambiwa kwamba Daudi amekwisha fika Keila, akasema: “Mungu amemutia katika mikono yangu maana amejifungia mwenyewe kwa kuingia katika muji wenye milango yenye vifungio.”


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις