Musikilize kelele kwenye milima kama za kundi kubwa la watu! Musikilize kelele za falme, na mataifa yanayokusanyika! Yawe wa majeshi analichunguza kundi linalokwenda kwa vita.
Nitatumia sheria kama kipimo changu, nitatumia haki kama timazi. Mvua ya mawe itaufagilia mbali uongo munaoutegemea, na mafuriko yataharibu kikingio chenu.
Silaha zote zilizotengenezwa kwa kukuzuru wewe hazitafaa kwa kitu chochote. Mutu akikushitaki, utamushinda. Hiyo ndiyo haki niliyowapangia watumishi wangu. Hizo ndizo haki nilizowahakikishia. –Ni ujumbe wa Yawe.
Muungane, enyi watu wa mataifa, na kufezeheshwa! Musikilize, enyi inchi za mbali katika dunia! Mujiweke tayari na kufezeheshwa. Mujiweke tayari na kufezeheshwa.
Maana mutoto amezaliwa kwa ajili yetu, tumepewa mutoto mwanaume. Naye atapewa mamlaka ya kutawala. Ataitwa: “Mushauri wa Ajabu”, “Mungu Mwenye Nguvu”, “Baba wa Milele”, “Mufalme wa Amani”.
Wameshika pinde zao na mikuki; ni watu wakali wasiokuwa na huruma. Vishindo vyao ni kama uvumi wa bahari. Wamepanda juu ya farasi, wamejipanga tayari kwa vita na wewe Sayuni!
Utukufu wa Mungu wa Israeli ulitokea upande wa mashariki. Pamoja nao kulikuwa mushindo wa kuja kwake kama mushindo wa maji mengi, inchi ilingaa kwa utukufu wake.
Kila wakati sanduku liliposafiri kwenda mbele, Musa alisema: Inuka, ee Yawe, uwatawanye waadui zako, na hao wanaokuchukia uwafanye wakimbie kutoka mbele yako.
“Vitambulisho vitaonekana katika jua, mwezi na nyota. Na hapa katika dunia mataifa yatakuwa na uchungu, na kushikwa na wasiwasi kwa ajili ya mungurumo na musukosuko wa bahari.
Halafu mumoja wa wale wamalaika saba walioshika vile vikombe saba akajongea na kuniambia: “Kuja nitakuonyesha namna gani yule kahaba mukubwa atakavyohukumiwa, ndio ule muji uliojengwa katikati ya mito mingi.