Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Isaya 16:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Kisha utawala wa wema utazinduliwa katika hema ya Daudi. Mutawala atakuwa mwaminifu. Atahukumu kufuatana na sheria ya Mungu, atakuwa mwepesi wa kutenda kwa haki.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Isaya 16:5
31 Σταυροειδείς Αναφορές  

Mungu wa Israeli amesema, Yeye Jiwe la Kufichamia la Israeli ameniambia: Mutu anayetawala watu kwa haki, anayewatawala akimwogopa Mungu,


Daudi alikaa kwenye kikingio hicho. Akakiita: “Muji wa Daudi.” Daudi akaongeza muji, akianzia uwanja wa Milo kuelekea ndani.


Ukoo wako na ufalme wako vitadumu imara siku zote. Kiti chako cha kifalme kitakuwa imara milele.”


Asifiwe Yawe, Mungu wako, ambaye amependezwa nawe, akakuweka juu ya kiti cha kifalme cha Israeli! Kwa sababu Yawe anapenda Israeli milele, amekuweka wewe ukuwe mufalme, kusudi uimarishe haki na sheria ya Mungu.”


Hivi ndivyo mufalme Hezekia alivyotenda mambo mema, ya haki na ya uaminifu mbele ya Yawe, Mungu wake, katika inchi yote ya Yuda.


Hakika yeye ni tayari kuwaokoa wanaomuheshimu, na utukufu wake utadumu katika inchi yetu.


Mukono wako unajaa nguvu, mukono wako una nguvu na umeshinda!


mbele ya Yawe kwa sababu anakuja. Anakuja kuhukumu dunia. Atahukumu dunia kwa haki, na mataifa kwa uaminifu wake.


Mushangilie mbele ya Yawe, maana anakuja kutawala dunia. Atahukumu ulimwengu kwa haki, atatawala mataifa kama vile inavyofaa.


Ee mufalme mukubwa, mupenda haki, umesimamisha usawa katika Israeli; umeleta sheria na haki.


Wema na uaminifu unamukinga mufalme; utawala wake unaimarishwa kwa haki.


Mufalme anayewaamua wamasikini kwa haki, ataona utawala wake unaimarika milele.


Maana Yawe ni mwamuzi wetu, yeye ni mutawala wetu; Yawe ni mufalme wetu, yeye ndiye anayetuokoa.


Mimi nilimufanya kuwa mukubwa na mutawala wa mataifa kusudi yeye anishuhudie kwa watu wa mataifa.


Akapewa mamlaka, utukufu na ufalme, kusudi watu wa makabila yote, mataifa yote na luga zote wamutumikie. Utawala wake ni wa milele na ufalme wake hautaangamizwa hata kidogo.


Ufalme, utawala na ukubwa wa falme zote katika dunia watapewa kwa watu wa watakatifu wa Mungu Mukubwa. Ufalme wao utakuwa wa kudumu milele, na tawala zote zitawatumikia na kuwatii.


Siku inakuja nitakapoisimika nyumba ya Daudi iliyoanguka; nitazitengeneza kuta zake, na kusimika upya mabomoko yake. Nitaijenga upya kama ilivyokuwa tangu zamani.


Hao waliolemewa ndio watakaobaki wazima; hao waliopelekwa katika uhamisho watakuwa taifa lenye nguvu. Yawe atawatawala kwenye mulima Sayuni, tangu wakati ule na hata milele.


Mushangilie sana enyi watu wa Sayuni! Mupige vigelegele, enyi watu wa Yerusalema! Angalia, mufalme wenu anawakujia, anakuja kwa shangwe na ushindi! Ni mupole, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, mutoto wa punda.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις