Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Isaya 15:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Moyo wangu unaugua kwa ajili ya inchi ya Moabu; wakimbizi wake wanakimbilia Zoari, wanakimbia mpaka Egilati-Selisiya. Wanapanda njia ya kwenda Luhiti wakilia, katika njia kwenda Horonaimu wanatoa kilio cha maangamizi.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Isaya 15:5
23 Σταυροειδείς Αναφορές  

Loti akainua macho yake, akaona bonde la muto Yordani, akaona kwamba lina maji ya kutosha kila pahali, kama vile bustani ya Yawe na kama vile inchi ya Misri upande wa Soari. (Hii ilikuwa mbele Yawe hajaiangamiza miji ya Sodoma na Gomora).


wakapigana vita na Bera mufalme wa Sodoma, na Birsa mufalme wa Gomora, Sinabu mufalme wa Adima, Semeberi mufalme wa Seboimu, na mufalme wa Bela ni kusema Soari.


Harakisha! Kimbilia kule, nami sitafanya lolote mpaka utakapofika kule.” Hivyo muji ule ukaitwa Soari.


Daudi alipokuwa akipita pamoja na watu wake, watu wote katika inchi yote walilia kwa sauti. Mufalme Daudi akavuka kijito cha Kidroni pamoja na watu wote, wakapita kuelekea katika jangwa.


Lakini Daudi aliendelea, akapanda kwenye mulima wa Mizeituni akilia, bila viatu na kichwa chake kimefunikwa. Hata watu wote waliokuwa pamoja naye walifunika vichwa vyao, wakapanda mulima wakilia.


Lakini sasa Yawe anasema hivi: Nyuma ya miaka mitatu kamili, ikihesabiwa kama vile mutumishi anavyohesabu siku zake, utukufu wa Moabu utapunguka. Ingawa watu wake ni wengi, watakaobaki wazima watakuwa wachache na wazaifu.


Maana leo Yawe wa majeshi ametuletea fujo, kushindwa na wasiwasi katika Bonde la Maono. Kuta za muji zimebomolewa. Kilio cha wakaaji wake kinasikilika mpaka kwenye milima.


Muko mbio kutenda maovu, muko wepesi kumwanga damu isiyokuwa na kosa. Mawazo yenu ni mawazo ya uovu, popote munapokwenda munaacha ukiwa na uharibifu.


Na kama musiponisikiliza, moyo wangu utalia machozi kwenye uficho, kwa sababu ya kiburi chenu. Nitalia kwa uchungu na kutoa machozi, maana watu wa Yawe wanapelekwa katika uhamisho.


Sikukukaza kutenda mabaya, wala sikutamani ile siku ya hasara ifike. Wewe mwenyewe unajua maneno niliyosema mbele yako.


Uchungu, uchungu! Ninagaagaa kwa uchungu! Moyo wangu unapigapiga vibaya. Wala siwezi kukaa kimya. Maana ninaogopa mulio wa baragumu, ninasikia kelele la vita.


Wanatangaza hasara zisizokoma; inchi yote imeharibiwa. Kwa rafla mahema yetu yameharibiwa, mapazia yao yamepasuka kwa dakika moja.


Sikiliza! Kilio kutoka Horonaimu: Maangamizi na uharibifu mukubwa!


Wale wanaopanda kwenda Luhiti wanalia kwa sauti. Wanapoteremuka kwenda Horonaimu, wanasikia kilio cha uharibifu.


Kwa kishindo cha kutekwa kwa Babeli, dunia itatetemeka, na kilio chake kitasikilika kati ya mataifa mengine.


Yawe anasema: Nitaifanya Yerusalema kuwa mabomoko matupu, nitaifanya kuwa pango la mbweha; na miji ya Yuda nitaifanya kuwa jangwa, pahali pasipokaliwa na mutu yeyote.


Ole wenu watu wa Moabu! Mumeangamizwa, enyi watu wa mungu Kemosi! Umewafanya watoto wenu wanaume kuwa wakimbizi, wabinti zako umewaacha watwaliwe mateka mpaka kwa Sihoni, mufalme wa Amori.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις