Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Isaya 13:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Yawe anasema hivi: Nitauazibu ulimwengu kwa uovu wake, waovu kwa sababu ya makosa yao. Nitakikomesha kiburi cha wenye majivuno, na kuporomosha mazarau ya watu wakali.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Isaya 13:11
30 Σταυροειδείς Αναφορές  

Umwangalie kila mwenye kiburi na kumuporomosha, uwakanyage waovu pahali wanapokuwa.


Ikiwa mwenye haki anapata malipo hapa katika dunia, hakika mwovu na mwenye zambi watalipwa!


Kumwogopa Yawe ni kuchukia uovu. Ninachukia kiburi, majivuno maisha mabaya, na luga mbaya.


Atawaamulia wamasikini kwa haki na kutetea haki za wakosefu katika inchi. Kwa neno lake dunia itaazibiwa, kwa pumzi yake waovu watauawa.


Mujitayarishe kuwachinja watoto wake kwa sababu ya makosa ya baba zao, wasipate kuamuka na kukamata inchi, na kuijaza dunia yote miji yao.


Yawe amelivunja gongo la waovu, ameivunja fimbo ya kifalme ya watawala,


Macho yenye kiburi ya wanadamu yatanyenyekezwa, watu wenye majivuno watashushwa chini, na Yawe peke yake atatukuzwa siku hiyo.


Kweli, siku ya Yawe wa majeshi inakuja juu ya wote wenye kiburi na majivuno, juu ya wote wanaojitukuza,


Kiburi cha wanadamu kitashushwa, majivuno ya watu yatanyenyekezwa, na Yawe peke yake atatukuzwa siku hiyo.


Yawe wa majeshi alinifunulia haya akisema: Hakika uovu huu hautasahauliwa mbele ya kufa kwenu. Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.


Ni Yawe wa majeshi! Yeye ndiye aliyeyapanga haya yote. Alifanya hivyo akiharibu kiburi chao na kuwapatisha haya waheshimiwa wake.


Siku ile Yawe ataliazibu jeshi la anga vilevile na wafalme wa dunia.


Kwa hiyo watu wenye nguvu watakutukuza, miji ya mataifa kali itakuogopa.


ni kama joto la jua juu ya inchi kavu. Lakini wewe unakomesha fujo ya wageni. Kama wingu linavyofifisha joto la jua, ndivyo unavyokomesha nyimbo za ushindi za watu wakali.


Maana Yawe anakuja kutoka kwake juu, kutoka makao yake huko mbinguni; kuwaazibu wakaaji wa dunia kwa uovu wao. Nayo dunia haitaficha tena wale waliouawa, lakini itaufichua umwagaji wa damu wote.


Watesaji watatoweka, wenye kumuchekelea Mungu watakwisha, wote wanaokusudia kutenda maovu watateketezwa.


Kundi la waadui zako litakuwa kama mavumbi laini, waliokutendea ukali watakuwa kama maganda. Hayo yatafanyika kwa rafla.


Lakini ole kwao watu waovu! Mambo yatawaendekea vibaya, maana yale waliyotenda yatawapata wao wenyewe.


Kila mutu atafezeheshwa, na wenye kiburi wote watapatishwa haya.


Nitawalipiza maovu yao wayalipe vilevile maovu ya babu zao. –Ni Yawe anayesema hivyo.– Wao waliifukizia ubani miungu yao kwenye milima, wakanitukana mimi kule juu ya vilima. Nitawalipa sawa inavyostahili, watayalipa matendo yao ya zamani.


Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu; Moabu ana majivuno sana. Tumesikia juu ya kujiona, kiburi na majivuno yake; tumesikia jinsi anavyojisifu ndani ya moyo.


Na sasa, mimi Nebukadneza ninamusifu na kumutukuza na kumuheshimu Mufalme wa mbinguni. Maana matendo yake yote ni ya haki, naye anawashusha wenye kiburi.


Andika: Uwaangalie wenye kiburi, hao wataangamia; lakini wenye haki wataishi kwa kumwamini Mungu.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις