Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Isaya 12:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Mumwimbie Yawe sifa maana ametenda mambo makubwa; haya yajulikane katika dunia yote.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Isaya 12:5
16 Σταυροειδείς Αναφορές  

Mushangilie, mumwimbie Mungu sifa, mueleze matendo yake ya ajabu!


Jina lake tukufu litukuzwe milele; utukufu wake ujae katika ulimwengu wote! Amina, Amina!


Zaburi. Mumwimbie Yawe wimbo mupya, kwa maana ametenda mambo ya ajabu! Nguvu yake kubwa, mukono wake mutakatifu umemupatia ushindi.


Kisha, Musa pamoja na Waisraeli wakamwimbia Yawe wimbo huu: “Nitamwimbia Yawe, maana ameshinda kwa utukufu; farasi na mupanda-farasi wake amewatupa katika bahari.


Miriamu akawaongoza kwa kuimba: “Mumwimbie Yawe maana ameshinda kwa utukufu. Farasi na mupanda-farasi wake amewatupa ndani ya bahari.”


Watu wanalalamika, wanaimba kwa shangwe. Kutoka upande wa magaribi, wanatangaza ukubwa wa Yawe,


Kwenda juu ya mulima murefu, ewe Sayuni, utangaze habari njema. Lalamika kwa nguvu, ewe Yerusalema, utangaze habari njema. Lalamika bila kuogopa. Uambie miji ya Yuda: Muangalie: Mungu wenu!


Mumwimbie Yawe wimbo mupya! Dunia yote iimbe sifa zake: bahari na vyote vinavyokuwa ndani yake, inchi za mbali na wakaaji wake;


jangwa na miji yake yote vipige kelele, vijiji vya wakaaji wa Kedari vimusifu, wakaaji wa Sela waimbe kwa shangwe; wapige kelele kutoka juu kwenye mulima.


Muimbe kwa furaha enyi mbingu, kwa sababu ya yale Yawe aliyotenda. Mupige kelele enyi vilindi vya dunia! Mupige vigelegele enyi milima! Enyi mapori na miti yote inayokuwa ndani yake, mushangilie. Maana Yawe amewakomboa wazao wa Yakobo, naye atatukuzwa katika inchi ya Israeli.


Utukufu wa Yawe utaenea pote katika dunia, kama vile maji yanavyoenea katika bahari.


Watu wa mataifa katika dunia yote tokea upande jua linapopanda mpaka upande jua linaposhuka wanalitukuza jina langu. Kila pahali wananifukizia ubani na kunitolea sadaka zinazokubaliwa; maana jina langu linatukuzwa kati yao.


Waliimba wimbo wa Musa, mutumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwana- Kondoo wakisema: “Ewe Bwana wetu, Mungu Mwenye Uwezo, matendo yako ni makubwa na ya ajabu! Ewe Mufalme wa mataifa, kazi zako ni za haki na za kweli!


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις