Kisha mufalme wa Asuria akapeleka watu kutoka Babeli, Kuta, Awa, Hamati na Sefarwaimu na kuwaweka katika miji ya Samaria kwa pahali pa watu wa Israeli waliopelekwa katika uhamisho. Wakaitwaa miji hiyo na kukaa mule.
Ni mungu gani kati ya miungu ya mataifa yale yaliyoharibiwa kabisa na babu zangu aliyeweza kuwakomboa watu wake kutoka katika mikono yangu ndiyo nanyi mukuwe na tumaini kwamba Mungu wenu atawaokoa toka mikono yangu?
Nyuma ya haya yote mufalme Yosia aliyofanya kwa ajili ya hekalu, Neko, mufalme wa Misri akapanda kwenda kushambulia Karkemisi kwenye muto Furati. Naye mufalme Yosia akatoka kwa kumushambulia,
Pango za Efuraimu zitatoweka, na utawala wa Damasiki utakwisha. Waaramu ambao watabaki wazima, hawatakuwa na utukufu zaidi kama wazao wa Israeli. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.
Barabara kubwa zimebaki tupu; hakuna anayesafiri kupitia ndani yao. Mapatano yanavunjwa ovyo, washuhuda wanazarauliwa. Hakuna anayejali tena maisha ya wanadamu.
Maana muji mukubwa wa Aramu ni Damasiki, na huyo Resini ni mukubwa wa Damasiki tu. Muji mukubwa wa Efuraimu ni Samaria, na mwana wa Remalia ni mukubwa wa Samaria tu. Katika miaka makumi sita na mitano utawala wa Efuraimu utavunjwa; Efuraimu halitakuwa taifa tena. Kama hautaamini, hautaimarika.
Juu ya Misri na jeshi la Neko mufalme wa Misri, lililokuwa huko Karkemisi karibu na muto Furati ambalo Nebukadneza mufalme wa Babeli alilishambulia katika mwaka wa ine wa utawala wa Yoyakimu mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda:
Hii ni juu ya Damasiki: Miji ya Hamati na Arpadi, imejaa wasiwasi kwa kufikiwa na habari mbaya; mioyo ya watu wake inayeyuka kwa hofu, imefazaika kama bahari isiyoweza kutulia.
Kutoka hapo utaendelea mpaka Berota na Sibraimu (unaokuwa kati ya Damasiki na Hamati), na mpaka muji wa Hazori-Hatikoni unaokuwa katika inchi ya Haurani.