Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Isaya 10:30 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

30 Enyi watu wa Galimu, mupige kelele! Enyi watu wa Laisi, mutege sikio! Enyi wenyeji wa Anatoti, mujibu!

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Isaya 10:30
9 Σταυροειδείς Αναφορές  

Mufalme Solomono akamwambia kuhani Abiatari: “Ondoka uende katika shamba lako, kule Anatoti. Unastahili kufa wewe. Lakini sasa, sitakuua kwa sababu ulilishugulikia Sanduku la Agano la Yawe ulipokuwa na baba yangu Daudi, ukateswa pamoja naye.”


Wengine walikaa Anatoti, Nobu, Anania,


Watu wa Madimena wamekimbia, wakaaji wa Gebimu wanatafuta makimbilio.


Maneno ya Yeremia mwana wa Hilkia, mumoja wa makuhani wa muji Anatoti, katika inchi ya kabila la Benjamina.


Kisha binamu yangu Hanameli akanifikia katika baraza la walinzi kama alivyonifahamisha Yawe, akaniambia: Nunua shamba langu linalokuwa kule Anatoti katika inchi ya Benjamina maana wewe uko na haki ya kulikomboa. Ulinunue kwa faida yako. Basi nikajua kwamba neno hili ni la Yawe.


Anatoti pamoja na mbuga zake za malisho, Almoni pamoja na mbuga zake za malisho. Jumla ya miji waliyopewa ni mine.


Walibadilisha jina la muji ule, wakauita Dani, kufuata jina la babu yao aliyekuwa mwana wa Israeli. Lakini muji ule pale mbele uliitwa Laisi.


Basi, watu hao watano wakaondoka, wakaenda Laisi. Waliwaona watu walioishi kule, na jinsi walivyokaa kwa usalama kama vile watu wa Sidona. Walikuwa watu watulivu wasiokuwa na wasiwasi na hawakupungukiwa mahitaji yoyote katika inchi. Walikuwa mbali na watu wa Sidona, na hawakukuwa na shuguli yoyote na watu wengine.


Wakati huo, Saulo alikuwa amemwoesha binti yake Mikali, ambaye alikuwa muke wa Daudi, kwa Palti mwana wa Laisi, wa muji wa Galimu.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις