Isaya 1:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
1 Haya ni maono Isaya mwana wa Amozi, aliyoyaona juu ya inchi ya Yuda na Yerusalema, katika nyakati za utawala wa wafalme hawa wa Yuda: Ahazi na Hezekia.
Katika mwaka wa makumi tatu na tisa wa utawala wa mufalme Azaria wa Yuda, Salumu mwana wa Yabesi akaanza kutawala Israeli na akatawala akiwa kule Samaria kwa muda wa mwezi mumoja.
Aliwaamuru Eliakimu, musimamizi wa nyumba ya kifalme, Sebuna mwandishi, na wazee wa makuhani, wamwendee nabii Isaya mwana wa Amozi, wakiwa wamevaa nguo za magunia.
Kisha watu wote wa Yuda wakamukamata Uzia mwana wa Amazia akiwa mwenye umri wa miaka kumi na sita, wakamufanya kuwa mufalme pahali pa Amazia baba yake.
Yotamu alikuwa na umri wa miaka makumi mbili na mitano alipoanza kutawala, alitawala kwa muda wa miaka kumi na sita kule Yerusalema. Mama yake aliitwa Yerusa binti ya Sadoki.
Ahazi alianza kutawala akiwa na umri wa miaka makumi mbili, alitawala kwa muda wa miaka kumi na sita kule Yerusalema. Yeye, hakufuata mufano muzuri wa Daudi babu yake, lakini alitenda maovu mbele za Yawe,
Miaka mitatu mbele ya pale, Yawe alimwambia Isaya mwana wa Amozi hivi: Kwenda uvue nguo ya gunia uliyokuwa umevaa katika kiuno, na viatu vyako. Isaya akafanya kama alivyoambiwa; akakuwa anatembea uchi na bila viatu.
Nimeonyeshwa maono ya kutisha: wadanganyifu wanadanganya na waangamizaji wanaangamiza. Mupande kwa kupigana vita, enyi Waelamu! Mushambulie, enyi Wamedi! Mungu atakomesha mateso yote yaliyoletwa na Babeli.
Aliwaamuru Eliakimu, musimamizi wa nyumba ya kifalme, Sebuna, katibu, na wazee wa makuhani, wamwendee nabii Isaya mwana wa Amozi, wakiwa wamevaa nguo za magunia.
Wakati ule, Hezekia aligonjwa sana karibu kufa. Halafu nabii Isaya mwana wa Amozi akamwendea, akamwambia: Yawe anasema hivi: Panga mambo yako sawasawa katika nyumba yako kwa sababu utakufa, hautapona.
Kwenda juu ya mulima murefu, ewe Sayuni, utangaze habari njema. Lalamika kwa nguvu, ewe Yerusalema, utangaze habari njema. Lalamika bila kuogopa. Uambie miji ya Yuda: Muangalie: Mungu wenu!
Katika mwaka mufalme Uzia alipokufa, nilimwona Bwana katika maono akiikaa katika kiti cha kifalme kinachoinuka juu sana. Pindo la nguo yake lilienea katika hekalu lote,
Katika siku za utawala wa Ahazi mwana wa Yotamu na mujukuu wa Uzia, wa inchi ya Yuda, Resini, mufalme wa Aramu, na Peka mwana wa Remalia, mufalme wa Israeli, walienda kuushambulia Yerusalema, lakini hawakuweza kuunyanganya.
Yawe wa majeshi anasema hivi: Musisikilize maneno manabii wanaowatabiria; wanawapa matumaini ya uongo. Yale wanayowaambia ni maono ya mioyo yao wenyewe. Hayakutoka katika kinywa cha Yawe.
Kwa siku ya tano ya mwezi wa ine, mwaka wa makumi tatu, wakati nilipokuwa katikati ya wale watu waliopelekwa katika uhamisho, karibu na muto Kebari, mbingu zikafunguka, nikapata maono toka kwa Mungu.
Hili ni neno ya Yawe lililomufikia Hosea mwana wa Beri katika siku za utawala wa Uzia, Yotamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda, na Yeroboamu mwana wa Yoasi, mufalme wa Israeli.
Haya ni maneno ya Amosi, mumoja wa wachungaji wa nyama wa muji wa Tekoa. Mungu alimufunulia Amosi mambo haya yote juu ya inchi ya Israeli miaka miwili mbele ya tetemeko la inchi, wakati Uzia alipokuwa mufalme wa Yuda, na Yeroboamu mwana wa Yoasi alipokuwa mufalme wa Israeli.
Mutoe sadaka ya shukrani ya mikate isiyotiwa chachu. Mutangaze popote kwamba mumetoa kwa mapenzi; maana ndivyo munavyopenda kufanya! –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
Hili ni neno la Yawe lilomufikia Mika, wa muji wa Moreseti wakati Yotamu, Ahazi na Hezekia walipokuwa wafalme wa Yuda. Mika aliona mambo yote haya juu ya Samaria na Yerusalema.
mashairi ya mutu aliyesikia maneno ya Mungu, na mutu anayejua maarifa ya Mungu Mukubwa, mutu anayeona maono ya Mungu Mwenye Nguvu, mutu anayeinama uso mpaka chini, macho wazi.
Petro alipokuwa angali na wasiwasi, naye akijiuliza juu ya maana ya maono yale, wale watu waliotumwa na Kornelio wakafika mbele ya mulango kwa maana walikuwa wamekwisha kujulishwa nafasi gani kunapokuwa nyumba ya Simoni.