Walipofika katika uwanja wa kupepetea ngano wa Atadi, ngambo ya muto Yordani, waliomboleza kwa huzuni kubwa, naye Yosefu akamufanyia baba yake marehemu kilio cha siku saba.
Kwa hiyo wakati wa mavuno nitaitwaa ngano yangu, nitaiondoa divai yangu kwa wakati wake. Nitamunyanganya nguo zangu za sufu na kitani, ambazo zilitumika kuufunika uchi wake.
Atawafuata wapenzi wake, lakini hatawapata; atawatafuta, lakini hatawaona. Kwa hiyo atasema: Nitarudi kwa mume wangu wa kwanza; maana zamani nilikuwa na raha kuliko sasa.
Ninyi munawagandamiza wazaifu na kuwalipisha kodi ya ngano. Munajijengea nyumba za mawe ya kuchongwa, lakini ninyi hamutaishi humo; munalima bustani nzuri za mizabibu, lakini hamutakunywa divai yake.
Mulitazamia mavuno mengi, lakini mulipata kidogo tu. Mulipoyaleta kwenye nyumba, niliyapeperusha mbali. Kwa nini? Kwa sababu nyumba yangu ni mabomoko matupu wakati kila mumoja wenu anashugulikia nyumba yake.
hali yenu ilikuwa namna gani? Mutu alifika kwenye fungu la ngano akingojea kupata vipimo makumi mbili, lakini kulikuwa vipimo kumi tu. Mutu alifika kwenye mutungi wa divai akingojea kujaza vyombo makumi tano, lakini kulikuwa makumi mbili tu.