Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Hosea 7:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Kwenye sikukuu ya mufalme, waliwalewesha sana wakubwa wake; naye mufalme akashirikiana na watu wa ovyoovyo.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Hosea 7:5
20 Σταυροειδείς Αναφορές  

Ilipotimia siku ya tatu, ambayo ilikuwa siku ya kufanya sikukuu ya kuzaliwa kwake, mufalme wa Misri akafanyia watumishi wake wote karamu. Akatoa katika kifungo mutunza vinywaji wake mukubwa na mupishi mukubwa wa mikate, akawaweka mbele ya wakubwa wake.


Mufalme Yeroboamu aliposikia maneno hayo ya mutu wa Mungu juu ya mazabahu kule Beteli, alinyoosha mukono akasema: “Mumukamate mutu yule!” Na mara moja ule mukono wake aliounyoosha, ukakauka, hakuweza tena kuukunja.


Heri mutu asiyefuata shauri la waovu, asiyeshiriki katika njia ya wenye zambi, wala kukusanyika na wenye kuzarau;


Nilipovaa gunia kwa kuomboleza, nikageuka kuwa wimbo kwao.


Anayeandamana na wenye hekima anapata hekima, lakini anayejiunga na wapumbafu atapata hasara.


Divai inaleta mazarau na kileo kinaleta ugomvi; yeyote anayevutwa navyo hana hekima.


Ole wa Samaria, muji unaokuwa kama taji juu ya bonde kwenye udongo muzuri. Walevi wa ajabu wa Efuraimu wanajivuna kwa ajili yake, lakini utukufu wake utatoweka kama ua linalonyauka!


Basi, musikilize neno la Yawe, enyi wenye mazarau munaotawala watu wa Yerusalema:


Pahali pake umejitukuza mwenyewe mbele ya Bwana wa mbinguni: umeleta vyombo vya nyumba ya Mungu ukavitumia kwa kunywea divai, wewe, wakubwa wako, wanawake wako na wahabara wako, na kuisifu miungu iliyotengenezwa na feza, zahabu, shaba, chuma, miti na mawe; miungu ambayo haioni, haisikii wala haijui jambo lolote. Lakini Mungu, ambaye uzima wako uko katika mukono wake, na njia zako ziko wazi mbele yake, haukumuheshimu!


Wanamufurahisha mufalme, lakini ni waovu; wanawafurahisha wakubwa, lakini ni wanafiki.


Na ilikuwa kwa sikukuu ya kuzaliwa kwa Herode, binti ya Herodia akacheza mbele ya wote walioalikwa. Binti yule akamupendeza Herode sana


Siku moja Herodia alipata wakati wa kumwua Yoane. Ilikuwa sikukuu ya kuzaliwa kwa Herode, wakati alipofanya karamu kwa wasimamizi wa serikali yake, wakubwa wa waaskari na waheshimiwa wa Galilaya.


Musilewe divai kwa maana inaleta upotovu, lakini mujazwe na Roho.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις