Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Hosea 3:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Hivi ndivyo Waisraeli watakavyokuwa: watakaa kwa muda murefu bila mufalme au mukubwa; bila sadaka, wala nguzo za sanamu wala vyombo walivyotumia kwa kujua mapenzi ya Mungu.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Hosea 3:4
44 Σταυροειδείς Αναφορές  

Wakati ule Labani alikuwa amekwenda kukata manyoya ya nyama wake. Hivyo Rakeli akapata nafasi ya kuiba sanamu za miungu ya baba yake.


Rakeli alikuwa ametwaa zile sanamu, akazificha chini ya matandiko ya ngamia na kuketi juu yake. Labani akazitafuta katika hema lote; lakini hakuzipata.


Fimbo ya kifalme haitatoka kwa Yuda, wala bakora ya utawala kwenye miguu yake, mpaka atakapofika yule ambaye ni yake; ambaye mataifa yatamutii.


Daudi alikuwa amejifungia kizibao cha kuhani katika kiuno chake. Alicheza kwa nguvu zake zote mbele ya Yawe.


Tena, kusudi mufalme Yosia atimize sheria zote zilizoandikwa katika kitabu Kuhani Mukubwa Hilkia alichokipata katika nyumba ya Yawe, aliondoa wachawi, watabiri, miungu, sanamu za miungu pamoja na vyombo vingine vilivyotumika kwa kuabudu miungu ya uongo kutoka inchi ya Yuda na kutoka Yerusalema.


naye akatoka kwenda kukutana na mufalme Asa, akamwambia: “Unisikilize, ee Asa na watu wote wa kabila la Yuda na la Benjamina! Yawe yuko pamoja nanyi, ikiwa mutakuwa pamoja naye. Mukimutafuta, mutamupata, lakini mukimwacha, naye atawaacha.


Uwaambie wamutengenezee vitu hivi: kifuko cha kifua, kizibao, kanzu, na ingine yenye kupambwa vizuri, kofia na mukaba. Ndugu yako Haruni na wana wake watavaa nguo zile kusudi wanitumikie kama vile makuhani.


Watatengeneza kizibao cha kuhani kwa nyuzi za zahabu na sufu ya rangi ya samawi, zambarau na nyekundu, na kitani safi iliyosokotwa, na kupambwa vizuri.


Milango yake imezama ndani ya udongo, ameharibu na kuvunjavunja vifungio vyake. Mufalme na wakubwa wake wako katika uhamisho kati ya mataifa. Hakuna sheria tena, manabii wake hawapati tena maono kutoka kwa Yawe.


Lakini moto umetoka kwenye shina lake, ukayateketeza matawi na matunda yake. Matawi yake hayatakuwa na nguvu hata kidogo, wala hayatakuwa fimbo za kifalme. Huo umekuwa wimbo wa maombolezo; ndivyo unavyoimbwa siku zote.


Ninyi munasema ndani ya mioyo yenu: Tutakuwa kama mataifa mengine, kama makabila ya inchi ingine na kuabudu miti na mawe. Hayo munayofikiri ndani ya mioyo yenu hayatafanikiwa hata kidogo.


Ewe upanga, shambulia upande wa kuume, shambulia upande wa kushoto; elekeza chongo yako pande zote.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: tosha kitambulisho chako cha kifalme na taji yako, maana mambo hayatabaki kama yalivyokuwa. Wanaokuwa chini watanyanyuliwa, wanaokuwa juu watashushwa!


Waaskari wake watalichafua hekalu na kuta zake, watakomesha sadaka za kuteketezwa kwa moto za kila siku na kusimamisha kule katika hekalu chukizo linaloleta uharibifu.


Tangu wakati wa kukomeshwa kwa sadaka za kuteketezwa kwa moto za kila siku, ni kusema kutoka wakati ule chukizo linaloleta uharibifu litakaposimamishwa, itakuwa muda wa siku elfu moja mia mbili na makumi kenda.


Mutawala huyo atafanya mapatano imara na watu wengi kwa muda wa miaka saba. Kisha nusu ya muda huo atakomesha sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka zingine. Pahali pa juu katika hekalu patasimamishwa chukizo linaloleta uharibifu, nalo litabaki pale mpaka yule aliyemusimamisha atakapoangamizwa kama ilivyopangwa na Mungu.


Yuko wapi sasa mufalme wenu awaokoe? Wako wapi wale wakubwa wenu wawalinde? Ninyi ndio mulioomba: Utupatie mufalme na wakubwa watutawale.


Kwa hasira yangu mimi nikawapa mufalme, kisha nikamwondoa kwa kasirani yangu.


Kwa hiyo wakati wa mavuno nitaitwaa ngano yangu, nitaiondoa divai yangu kwa wakati wake. Nitamunyanganya nguo zangu za sufu na kitani, ambazo zilitumika kuufunika uchi wake.


Kisha akamuvalisha Haruni koti na kuifunga kwa mukaba, akamuvalisha kanzu, akamuvalisha kizibao na kukifunga kwenye kiuno chake kwa mukaba uliofumwa kwa ufundi.


Sanamu zao za kupigia ramuli ni uongo mutupu, na waaguzi wao wanaagua uongo; watabiri wao wanatabiri ndoto danganyifu, na kuwapa watu faraja za bure. Ndiyo maana watu wa Yuda wanatangatanga kama kondoo; wanataabika maana wamekosa muchungaji.


Wakati ule, nitaondoa majina ya sanamu za miungu katika inchi, wala hayatakumbukwa tena. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.– Na wanaojidai kuwa manabii nitawaondoa kabisa pamoja na tamaa zao za kuabudu sanamu.


Wamoja watauawa kwa vita na watapelekwa kuwa wafungwa katika inchi za mataifa yote. Vilevile mataifa mengine yatautawala Yerusalema mpaka nyakati zao za kuutawala zitakapokwisha.”


Lakini wakapiga kelele wakisema: “Umwue! Umwue! Umutundike juu ya musalaba!” Pilato akawauliza: “Munataka nimutundike mufalme wenu juu ya musalaba?” Wakubwa wa makuhani wakajibu: “Sisi hatuna mufalme mwingine isipokuwa Mufalme wa Roma.”


Kwa maana tukifanya zambi kwa makusudi tukisha kutambua waziwazi ukweli, hakuna tena sadaka ingine inayoweza kutolewa kwa ajili ya usamehe wa zambi zetu.


Mutu huyo, Mika alikuwa na pahali pake pa ibada. Alitengeneza kizibao cha kuhani na sanamu, kisha akamufanya mumoja wa watoto wake kuwa kuhani wake.


Watu wale watano waliokwenda kuipeleleza inchi ya Laisi wakawaambia wandugu zao: “Munajua kwamba katika nyumba moja kati ya hizi kuna kizibao, sanamu ya kuchongwa na sanamu yenye kuyeyushwa? Basi, mufikiri namna ya kufanya.”


Gideoni akazitumia kwa kutengenezea kizibao ambacho alikiweka kwenye muji wake wa Ofura. Waisraeli wote wakaenda kule kukiabudu. Kizibao hicho kikakuwa mutego kwa Gideoni na jamaa yake.


Ahiya mwana wa Ahitubu ndugu yake na Ikabodi mwana wa Finehasi mujukuu wa Eli kuhani wa Yawe katika muji wa Shilo, alikuwa ndiye aliyevaa kizibao cha kuhani. Watu hawakujua kwamba Yonatani amekwisha ondoka.


Uasi ni sawa na zambi ya kuaguza, na kiburi ni sawa na uovu wa kuabudu sanamu. Kwa sababu umeikataa amri ya Yawe, naye amekukataa kuwa mufalme.”


Wakati ule, kijana Samweli aliendelea kumutumikia Yawe, akiwa amevaa kizibao cha kitani.


Basi, Daudi akamwambia Ahimeleki: “Una upanga au mukuki ambao unaweza kunipatia? Kwa maana shuguli za mufalme zilinilazimisha niondoke haraka, nami niliondoka bila upanga wangu wala silaha nyingine yoyote.”


Kwa hiyo, mufalme Saulo akamwambia Doegi: “Wewe geuka uwaue makuhani.” Doegi Mwedomu akaenda na kuwaua makuhani wote. Siku hiyo, Doegi aliua makuhani makumi nane na watano ambao wanavaa vizibao vya kikuhani vya kitani.


Abiatari mwana wa Ahimeleki, alipokimbilia kwa Daudi kule Keila, alikwenda na kizibao cha kuhani.


Daudi aliposikia mipango miovu ya Saulo juu yake, akamwambia kuhani Abiatari: “Ulete hapa kile kizibao cha kuhani.”


Daudi akamwambia kuhani Abiatari mwana wa Ahimeleki: “Uniletee kizibao cha kuhani.” Abiatari akamupelekea.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις