Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Hosea 13:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Waefuraimu wanaendelea kutenda zambi, wanajitengenezea sanamu za feza yenye kuyeyushwa, sanamu zinazotengenezwa kwa ufundi wao, zote zikiwa kazi ya wafundi. Wanasema: Muzitambikie! Wanaume wanabusu sanamu ya mwana-ngombe!

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Hosea 13:2
33 Σταυροειδείς Αναφορές  

Lakini, nitawaacha wazima watu elfu saba katika inchi ya Israeli, ambao hawajainama mbele ya Bali, wala kuibusu sanamu yake.”


Wakawaambia: “Musiwalete humu wafungwa hao, kwa sababu munakusudia kutuletea kosa mbele ya Yawe, tendo hili huku litakuwa nyongezo ya zambi yetu na kosa letu; kwa sababu kosa letu tayari ni kubwa na kuna kasirani kali juu ya Israeli.”


Naye hakujinyenyekeza mbele za Yawe, kama vile Manase alivyofanya, lakini yeye aliongeza kutenda makosa zaidi.


Niwapige wapi tena, ninyi munaoendelea kuasi? Kichwa chote kinajaa vidonda, na moyo unaumia kabisa!


Ole watoto waasi, wanaotimiza mipango yao na si mipango yangu, wanaofanya mapatano kinyume cha mapenzi yangu! –Ni ujumbe wa Yawe.– Kweli, wanalundika zambi juu ya zambi.


Hakika wote wanaoshirikiana na sanamu watapata haya, tena hao wafundi wa sanamu ni wanadamu tu. Basi, wakutane wote, wajitokeze, nao wataogopa na kufezeheka.


Enyi watu wa mataifa muliobaki, mukusanyike pamoja mukuje! Ninyi mumekosa akili: ninyi munabeba sanamu za miti na kumwomba mungu asiyeweza kuokoa watu.


Watu wanapoteza zahabu kutoka mifuko yao, wanapima feza kwenye mizani zao, wanamulipa mufuaji wa zahabu awatengenezee sanamu ya mungu, kisha wanainama mbele yake na kuiabudu!


Mukumbuke jambo hili na kufikiri, mujiulize ndani ya mioyo yenu enyi waasi.


Kisha watu wanaipamba kwa feza na zahabu wakiipigilia misumari na nyundo kusudi isianguke.


Wote ni wajinga na wapumbafu, fundisho la sanamu hizi ni mazarau matupu!


Mbona basi, watu hawa wameacha njia inayokuwa sawa na kuendelea katika upotovu wao? Wanashikamana na miungu yao ya uongo, na kukataa kunirudilia mimi!


Waisraeli walikuwa kama muzabibu muzuri, muzabibu wenye kuzaa matunda. Kadiri matunda yalivyozidi kuongezeka, ndivyo walivyozidi kujijengea mazabahu. Kadiri inchi yao ilivyozidi kustawi, ndivyo walivyozidi kupamba nguzo zao za ibada.


Wakaaji wa Samaria watatetemeka kwa sababu ya sanamu ya mwana-ngombe wa kule Beteli. Watu wake watamwombolezea mwana-ngombe yule, hata makuhani wanaomwabudu watamulilia; maana utukufu wa mwana-ngombe yule umeondolewa.


Lakini kadiri nilivyozidi kuwaita, ndivyo walivyozidi kwenda mbali nami; waliendelea kuyatambikia Mabali, na kuvifukizia ubani sanamu za miungu.


Upanga utavuma katika miji yao, utavunjavunja miimo ya milango yake na kuwaangamiza katika kuta zao.


Muombe huruma kwake, mumurudilie na kumwambia: Utusamehe uovu wote, upokee zawadi zetu, nasi tutakusifu kwa moyo.


Basi, nitafunga njia yake kwa miiba, nitamuzungushia ukuta, asipate njia ya kutokea inje.


Watu wa Efuraimu wamejiunga na sanamu. Basi! Uwaache waendelee tu!


Walijiwekea wafalme bila ruhusa yangu, walijichagulia wakubwa ambao sikuwatambua. Wamejitengenezea miungu ya feza na zahabu, jambo ambalo litawaangamiza.


Enyi watu wa Samaria, ninaichukia sanamu yenu ya mwana-ngombe. Hasira yangu inawaka juu yenu. Mutaendelea kuwa na makosa mpaka wakati gani?


Ile sanamu inatoka Israeli, ni fundi ndiye aliyeitengeneza. Yenyewe si Mungu hata kidogo. Kweli! Sanamu ya mwana-ngombe ya Samaria itavunjwavunjwa!


Na sasa, enyi kizazi cha wenye zambi, mumesimama kwa pahali pa wazee wenu, kuongeza tena hasira kali ya Yawe juu ya Waisraeli.


Lakini Mungu alimujibu namna gani? Alimwambia: “Nimejiwekea watu elfu saba waliokataa kupiga magoti mbele ya mungu Bali.”


Lakini wewe ni mugumu na mwenye moyo usiotaka kugeuka. Kwa hiyo unajiwekea azabu kubwa siku Mungu atakapoonyesha kasirani yake na hukumu yake ya haki.


Lakini watu waovu na wadanganyifu wataendelea katika maovu, wakipotosha watu wengine na kujipotosha wenyewe.


Halafu Samweli akatwaa chupa ndogo ya mafuta akamumiminia Saulo juu ya kichwa, akamubusu na kumwambia: “Yawe amekutia mafuta ukuwe mutawala juu ya watu wake.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις