Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Hosea 11:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Watu wangu wamekusudia kuniacha mimi, wakiitwa kusimama wapande juu, hakuna hata mumoja anayeweza.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Hosea 11:7
18 Σταυροειδείς Αναφορές  

Mbona basi, watu hawa wameacha njia inayokuwa sawa na kuendelea katika upotovu wao? Wanashikamana na miungu yao ya uongo, na kukataa kunirudilia mimi!


Inchi ya Asuria haitatuokoa, hatutategemea tena farasi wa vita. Hatutaziita tena Mungu wetu hizo sanamu tulizochonga. Kwako, ee Mungu, yatima anapata huruma.


Lakini kadiri nilivyozidi kuwaita, ndivyo walivyozidi kwenda mbali nami; waliendelea kuyatambikia Mabali, na kuvifukizia ubani sanamu za miungu.


Wanaigeukia miungu ya bure, wako kama upinde ulioregea. Waongozi wao watakufa kwa upanga, kwa sababu ya maneno yao ya kiburi. Kwa hiyo, watazarauliwa katika inchi ya Misri.


Yawe akaendelea kuniambia hivi: Muasi Israeli amejionyesha kuwa wa haki kuliko Yuda mudanganyifu.


Mutu mupotovu atavuna matunda ya mwenendo wake, naye mutu muzuri atapata malipo ya matendo yake.


Mimi ni Yawe, Mungu wako, niliyekutoa katika inchi ya Misri. Fungua kinywa chako, nami nitakulisha.


Waisraeli ni wenye kichwa kigumu kama punda. Kwa nini basi Mungu ashugulike na kuwachunga, kama kondoo katika shamba kubwa la kuwakulishia?


Nao watu wanasema: Ingawa zambi zetu zinatoa ushuhuda juu yetu, utusaidie ee Yawe kwa ajili ya heshima ya jina lako. Maasi yetu ni mengi, tumetenda zambi mbele yako.


Lakini waovu hata wakipewa rehema, hawawezi kujifunza kutenda haki. Hata katika inchi ya usawa, wao bado wanatenda maovu, wala hawajali ukubwa wako wewe Yawe.


Uovu wako utakuazibu; na uasi wako utakuhukumu. Ujue na kutambua kwamba ni vibaya sana kuacha Bwana wako Yawe, Mungu wako, na kutokuwa na woga wangu ndani yako. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi.–


Tangu siku ile babu zenu walipotoka Misri mpaka leo, sikuchoka kuwatuma kwenu manabii wote, watumishi wangu.


Lakini hawakunisikiliza wala kunitegea sikio, lakini wakazidi kufanya vichwa vyao kuwa vigumu na kuasi kuliko hata babu zenu.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις