Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Hesabu 16:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Wakakusanyika mbele ya Musa na Haruni, wakawaambia: Ninyi mumepitisha kipimo! Waisraeli wote pamoja ni watakatifu; kila mumoja ni mutakatifu. Yawe yuko pamoja nasi wote. Mbona sasa ninyi munajifanya wakubwa kushinda watu wengine wa Yawe?

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Hesabu 16:3
20 Σταυροειδείς Αναφορές  

Wayuda wanaoa wanawake wa kigeni na kuwaoea wana wao vilevile. Hivyo, taifa takatifu la Mungu limechanganyika na watu wa mataifa mengine. Vilevile wasimamizi na wakubwa ndio wa kwanza kutenda maovu hayo.”


Kule katika kambi walimwonea Musa wivu, na Haruni, mutumishi mutakatifu wa Yawe.


mbona unauonea kijicho mulima Mungu aliouchagua akae juu yake? Yawe atakaa huko milele!


Mutakuwa kwangu ufalme wa makuhani na taifa takatifu.’ Hayo ndiyo maneno utakayowaambia Waisraeli.”


watawapasha wakaaji wa inchi habari hii. Maana watu hawa wamekwisha kupata habari kwamba wewe, ee Yawe, uko pamoja nasi; maana wewe, ee Yawe, unaonekana waziwazi wingu lako linaposimama juu yetu, na kwamba wewe unatutangulia muchana kwa nguzo ya wingu na usiku kwa nguzo ya moto.


Si Haruni tu munayemunungunikia, wewe na kundi lako, lakini kwa kweli munamwasi Yawe.


muweke makaa ya moto ndani na kutia ubani juu yake, kisha mutavipeleka mbele ya Yawe. Halafu tutaona ni nani aliyechaguliwa na Yawe. Ninyi Walawi mumepitisha kipimo!


Yawe hajaona ubaya kwa watu wa Yakobo, wala uovu kwa hao watu wa Israeli. Yawe Mungu wao yuko pamoja nao, Yeye anasifiwa kwa vigelegele kati yao, yeye anapokea sifa zao za kifalme.


Musichafue inchi ambayo munakaa ndani yake, inchi ambayo mimi ninakaa ndani yake; maana mimi Yawe ninakaa kati yenu Waisraeli.


Mutawatoa inje ya kambi watu wote hawa, wanaume na wanawake, kusudi wasichafue kambi yangu ninamokaa.


“Babu zetu hawakutaka kumusikiliza Musa, wakamukataa na kutamani kurudi Misri.


“Ninyi watu wagumu! Ninyi wenye roho ya kipagani na masikio yanayofungana! Siku zote munapingana na Roho Mutakatifu sawa vile babu zenu walivyofanya!


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις