Pamoja na mwana-kondoo wa kwanza, utatoa kilo moja ya unga laini uliochanganywa na litre moja ya mafuta safi, na litre moja ya divai kama sadaka ya kinywaji.
Vilevile atatoa kikapu cha mikate isiyotiwa chachu: maandazi ya unga laini na mafuta, na mikate myembamba iliyopakwa mafuta pamoja na sadaka za vyakula na za kinywaji.
Uwaamuru Waisraeli maneno haya: Ninyi mutanitolea kwa wakati wake sadaka zinazotakiwa: vyakula vya kuteketezwa kwa moto, vyenye harufu nzuri ya kupendeza.
Lakini muzabibu ukajibu: ‘Munazani ninaweza kuacha shuguli yangu ya kuzalisha divai ambayo inafurahisha miungu na wanadamu, niende kujisumbua kuitawala miti?’
Wakamutolea Yawe sadaka. Kesho yake wakamutolea sadaka za kuteketezwa kwa moto: ngombe dume elfu moja, wana-kondoo elfu moja, pamoja na sadaka zao za vinywaji na sadaka nyingi kwa ajili ya Waisraeli wote.