Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Hesabu 15:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 mukinitolea mimi Yawe sadaka kutoka katika mifugo yenu, sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya kutimiza kiapo au kutoa sadaka ya mapenzi au sadaka ya wakati wa sikukuu zenu zilizowekwa, na kufanya harufu nzuri ya kunipendeza mimi Yawe,

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Hesabu 15:3
27 Σταυροειδείς Αναφορές  

Harufu nzuri ya sadaka hiyo ikamupendeza Yawe, naye akasema ndani ya moyo wake: “Sitailaani tena inchi hata kidogo kwa sababu ya mwanadamu. Ninajua kwamba mawazo yake ni maovu tangu utoto wake. Wala sitaangamiza tena viumbe vyote kama vile nilivyofanya.


Feza hiyo utaitumia kwa uangalifu sana kwa kununua ngombe dume, kondoo dume, wana-kondoo na sadaka ya unga na divai, na kuvitoa kwenye mazabahu katika nyumba ya Mungu wenu inayokuwa Yerusalema.


Ninajua Mungu ni musaada wangu, Yawe anaimarisha maisha yangu.


Kisha utamuteketeza kondoo muzima juu ya mazabahu kwa kunitolea sadaka ya kuteketezwa. Harufu ya sadaka inayotolewa kwa moto itanipendeza mimi Yawe.


Kisha utavitwaa tena kutoka mikono yao na kuviteketeza juu ya mazabahu pamoja na ile sadaka ya kuteketezwa, vikuwe harufu nzuri itakayonipendeza mimi Yawe. Hiyo ni sadaka inayotolewa kwa moto.


Vilevile na yule mwana-kondoo mwingine wa magaribi utamutolea sadaka pamoja na sadaka ya ngano na ya kinywaji kama vile ulivyofanya asubui. Harufu ya sadaka hiyo inayotolewa kwa moto itanipendeza mimi Yawe.


Mutaikula katika Pahali Patakatifu kwa sababu hiyo ni haki yako na wazao wako kutoka katika sadaka Yawe anazotolewa kwa moto. Hivi ndivyo nilivyoamuriwa.


Uwaambie Waisraeli hivi: Mutu akifanya kiapo cha kumutolea Yawe mwanadamu, mutu huyu anaweza kuondoa kiapo chake kwa kulipa kipimo cha feza kinachokadiriwa kama hivi:


Lakini kama sadaka hiyo ya amani ni ya kutimiza kiapo au ya mapenzi mema, itakuliwa siku hiyohiyo inapotolewa na sehemu ingine inaweza kukuliwa kesho yake.


Mutatoa sadaka ya kuteketezwa, harufu nzuri ya kumupendeza Yawe: wana-ngombe dume wawili, kondoo dume mumoja, na wana-kondoo dume saba wa mwaka mumoja, wote hao wakuwe bila kilema.


Mutamutolea Yawe sadaka ya kuteketezwa kwa moto, harufu ya kumupendeza Yawe: mwana-ngombe mumoja, kondoo dume mumoja, wana-kondoo saba wa mwaka mumoja. Wote wasikuwe na kilema.


Vilevile atatoa kikapu cha mikate isiyotiwa chachu: maandazi ya unga laini na mafuta, na mikate myembamba iliyopakwa mafuta pamoja na sadaka za vyakula na za kinywaji.


Na sauti ikasikilika toka mbinguni, ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa; ninapendezwa naye sana.”


Kwa maana sisi ni kama harufu nzuri iliyotolewa na Kristo kwa Mungu; na kunukia wale wanaookolewa na wale wanaopotea.


Kwa wale wanaopotea ni harufu ya kifo inayoleta kifo; lakini kwa wale wanaookolewa, ni harufu ya uzima inayoleta uzima. Basi nani anayekuwa na uwezo wa kutimiza kazi ya namna hii?


Muishi katika upendo kama vile Kristo alivyotupenda na kutoa maisha yake kwa ajili yetu kama vile matoleo na sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri inayomupendeza Mungu.


basi huko pahali Yawe, Mungu wenu, atakapochagua kusudi jina lake likae pale, hapo mutapeleka yote ninayowaamuru: sadaka zenu za kuteketeza kwa moto na sadaka zingine, sehemu ya kumi za mazao yenu, na sadaka za kutimiza kiapo.


Musikule vitu hivi pahali munapoishi: sehemu ya kumi za ngano zenu, divai zenu au mafuta yenu, wazaliwa wa kwanza wa ngombe wenu au kondoo wenu, au sadaka zenu za kutimiza kiapo au za mapenzi, au matoleo mengine.


Vilevile huko mutapeleka sadaka zenu za kuteketezwa kwa moto na sadaka zingine, sehemu ya kumi za mazao yenu, matoleo yenu ya mapenzi na ya kutimiza kiapo, na wazaliwa wa kwanza wa ngombe na kondoo wenu.


Kweli nina vitu vyote vya lazima na zaidi kupita. Sasa kwa kuwa Epafrodito ameniletea zawadi zenu zote, ninatosheka. Zawadi hizi ni kama sadaka ya ubani yenye harufu nzuri, na kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto inayokubaliwa na Mungu na kumupendeza.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις