Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Hesabu 12:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 (Musa alikuwa mutu munyenyekevu kuliko watu wengine wote waliokuwa katika dunia.)

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Hesabu 12:3
16 Σταυροειδείς Αναφορές  

Yawe anawashikilia wanyenyekevu, lakini anawaangusha waovu katika mavumbi.


Maana Yawe anapendezwa na watu wake; yeye anawaheshimisha wanyenyekevu kwa kuwapa ushindi.


Halafu kwa rafla, Yawe akawaambia Musa, Haruni na Miriamu: Mukuje katika hema la mukutano, ninyi watatu. Basi, wote watatu wakaenda kwenye hema la mukutano.


Mukubali kuongozwa nami kama vile ngombe dume anayefungiwa nira, nanyi mufuate mafundisho yangu maana mimi ni mupole na munyenyekevu. Kwa hiyo mutapumzika.


“Muwaambie wakaaji wa muji Sayuni: ‘Angalia, mufalme wenu anakuja kwenu. Yeye ni munyenyekevu, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, kitoto cha punda.’ ”


Heri wale wanaokuwa wapole, maana watarizi dunia!


Sasa mimi Paulo mwenyewe ninawaomba kwa upole na kwa wema sawa na ule wa Kristo; mimi yule ambaye wanasema juu yake kwamba ni mupole wakati ninapokuwa pamoja nanyi, lakini ni mukali wakati ninapokuwa mbali nanyi.


Ninazani kwamba wale mitume wanaohesabiwa kuwa wakubwa zaidi hawanipiti kitu kabisa.


Ninasema kama mupumbafu, lakini ni ninyi ndio mumenilazimisha kufanya vile. Kufuatana na ile, ningepaswa kusifiwa nanyi. Kwa maana hata kama mimi si kitu, wale mitume wenu wanaohesabiwa kuwa wakubwa hawanipiti kitu kabisa.


ijapokuwa sisi ni mitume wa Kristo, tungeweza kudai mambo fulani kwenu. Lakini sisi tulionyesha upole kati yenu kama vile mama anavyosumbuka kwa ajili ya watoto wake.


Nani anayekuwa na hekima na ufahamu kati yenu? Basi aonyeshe jambo lile kwa njia ya mwenendo wake muzuri, kwa njia ya matendo yanayofanyika katika upole unaotokana na hekima ile.


Lakini mapambo yenu yanapaswa kuwa ya ndani ya moyo yasiyoweza kuharibika. Sherti mapambo yale yakuwe yenye kutokana na roho ya amani na upole inayohesabiwa kuwa ya bei kali mbele ya Mungu.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις