Waisraeli watapiga kambi zao, kila mumoja akikaa pahali penye bendera yake, penye vitambulisho vya ukoo wake. Watapiga kambi zao kuzunguka na kuelekea hema la mukutano.
Hivi ndivyo, Waisraeli walivyofanya kila kitu kama vile Yawe alivyomwamuru Musa. Wakapiga kambi zao, kufuata bendera zao na wakasafiri kila mumoja akiandamana na jamaa yake kwa kufuata ukoo wake.