Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Esteri 9:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Nao viongozi wote wa majimbo, watawala, wakubwa na wakubwa wa mufalme vilevile waliwasaidia Wayuda, maana wote walimwogopa Mordekayi.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Esteri 9:3
9 Σταυροειδείς Αναφορές  

Viongozi wao walikuwa Zerubabeli, Yesua, Nehemia, Seraya, Relaya, Mordekayi, Bilsani, Misipari, Bigwayi, Rehumu na Bana. Hii ndiyo hesabu ya watu wote wa ukoo za Waisraeli waliorudi kutoka katika uhamisho:


Vilevile wakawapa wasimamizi wa mufalme na watawala wa mukoa wa majimbo ya upande wa magaribi wa muto Furati maagizo waliyopewa na mufalme, nao wakatoa musaada kwa watu na kwa ajili ya nyumba ya Mungu.


Basi, siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kwanza, Hamani akawaita waandishi wote wa mufalme, akawapa tangazo ambalo alitaka litafsiriwe kwa kila luga na kila namna ya maandiko katika utawala ule, na halafu mifano ya barua isambazwe kwa watawala wote, wakubwa wa majimbo yote, na viongozi wa makabila – kufuatana na luga zinazotumika kwao. Tangazo hilo likatolewa kwa jina la mufalme Ahasuero, na kupigwa muhuri kwa pete yake.


Katika kila jimbo na kila muji, popote pale tangazo hili liliposomwa, Wayuda wakafurahi na kushangilia, wakafanya sherehe na mapumziko; na watu wengine wengi wakajifanya kuwa Wayuda, maana waliwaogopa sana Wayuda.


“Ikikupendeza, ewe mufalme, na kama nimepata kukubaliwa mbele yako, ukiona ni vizuri nami nikikupendeza, tafazali, toa tangazo la kuvunja mipango ambayo Hamani alikuwa ameamuru itimizwe. Mipango hiyo ni ile ya mwana wa Hamedata, wa uzao wa Agagi, aliyopanga kwa kuwaangamiza Wayuda wote katika majimbo yote.


Basi, katika siku ya makumi mbili na tatu ya mwezi wa tatu inayoitwa Siwani, Mordekayi akawaita waandishi wote wa mufalme, akawaagiza waandike barua kwa Wayuda na wakubwa, watawala na wakubwa wa majimbo yote mia moja makumi mbili na saba, kuanzia Uhindi mpaka Etiopia. Barua hizo zikaandikwa kwa kila jimbo katika luga yake na sawasawa na maandiko yake, vilevile na kwa Wayuda kwa maandiko yao na luga yao.


Kisha mufalme akaamuru maliwali, wasimamizi, watawala, washauri, walinzi wa mali, waamuzi, wana sheria na wakubwa wote wa majimbo wahuzurie sikukuu ya kuzindua sanamu aliyosimamisha.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις