Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Esteri 7:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Harbona, mumoja wa wale matowashi waliomutumikia mufalme, akasema: “Hamani amesubutu hata kutengeneza muti wa kumutundikia Mordekayi ambaye aliyaokoa maisha yako, ewe mufalme. Muti huo, wenye urefu wa metre makumi mbili na mbili, bado uko kule katika nyumba yake.” Hapo mufalme akaamuru: “Mumutundike Hamani juu ya muti uleule.”

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Esteri 7:9
20 Σταυροειδείς Αναφορές  

Yehu akaangalia juu na kusema: “Ni nani anayekuwa upande wangu?” Wakubwa wawili au watatu wakatokeza vichwa vyao kwa kumwangalia kutoka kwenye dirisha,


Siku ya saba ya karamu hiyo, mufalme Ahasuero akiwa amejaa furaha kutokana na divai aliyokuwa amekunywa, akawaita matowashi saba waliomutumikia yeye mwenyewe: Mehumani, Bizita, Harbona, Bigita, Abagita, Zetari na Karkasi.


Basi, muke wake Zeresi na warafiki zake wakamushauria hivi: “Kwa nini asitengenezewe muti wa kutundikia, wenye urefu wa metre makumi mbili na mbili? Kesho asubui, unaweza kuzungumuza na mufalme kusudi Mordekayi auawe juu yake, kisha uende ukule karamu na mufalme kwa furaha.” Wazo hilo lilimufurahisha Hamani, naye akatengeneza muti ule.


Walipokuwa bado wanaongea juu ya hayo, matowashi wa mufalme wakafika kumutwaa Hamani kwenda kwenye karamu ya Esteri.


Ikaonekana jinsi ilivyoandikwa ikielezwa jinsi Mordekayi alivyopasha habari ya shauri la kumwua mufalme iliyokuwa imefanywa na Bigitani na Teresi, hao wawili kati ya matowashi wa mufalme waliokuwa walinzi wa vyumba vya mufalme.


Mufalme Ahasuero akawaambia malkia Esteri na Mordekayi, yule Muyuda: “Muangalie! Nimemupa Esteri mali ya Hamani, naye wamekwisha kumutundika kwa sababu ya shauri lake baya juu ya Wayuda.


Mufalme akaamuru hayo yatimizwe, na tangazo likatolewa katika muji Susani. Wana kumi wa Hamani wakatundikwa juu ya muti.


Lakini Esteri alipomwendea mufalme, naye mufalme akatoa amri kwa waandishi kwamba lile shauri baya ambalo Hamani alikuwa amefanya juu ya Wayuda, limurudilie yeye mwenyewe; na ya kuwa yeye na wana wake wauawe kwa kutundikwa kwenye muti.


Waovu wanaswe katika mitego yao wenyewe, wakati mimi ninaponyoka.


Maangamizi yawapate wao kwa rafla, wanaswe katika mutego wao wenyewe, watumbukie katika shimo lao wenyewe!


Wanaangamizwa kwa rafla, wateketezwe kabisa kwa vitisho.


Kwa hiyo mufalme akafurahi sana; akaamuru kwamba wamwondoe Danieli toka ndani ya pango. Basi wakamwondoa, naye hakuonekana na alama hata kidogo ya kidonda, kwa sababu alimutegemea Mungu wake.


Basi, hao wakubwa na maliwali wote pamoja, wakamwendea mufalme na kumwambia: Uishi milele ee mufalme Dario!


Basi, akaenda mbio, akasimama juu ya Goliati, akachomoa upanga wa Goliati toka katika mufuko wake, akamwua Goliati kwa kumukata kichwa chake. Wafilistini walipoona kwamba shujaa wao ameuawa, wakakimbia mbio.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις