Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Esteri 6:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Usiku ule, mufalme hakupata usingizi. Basi, akaamuru kitabu cha Mambo ya Siku cha matukio ya kila siku, kiletwe, nacho kikasomwa mbele yake.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Esteri 6:1
12 Σταυροειδείς Αναφορές  

Kwa hiyo, Abrahamu akapaita pahali pale: “Yawe anajalia,” kama inavyosemwa hata leo: “Kwa mulima wa Yawe, watu wanajaliwa.”


Matendo yake yote makubwa na ya ajabu, pamoja na simulizi kamili juu ya jinsi alivyomupandisha Mordekayi cheo na kumupatia heshima kubwa, yote yameandikwa katika kitabu cha Mambo ya Siku cha ufalme wa Media na Persia.


Wakati Mordekayi alipokuwa anaikaa kwenye mulango wa mufalme, Bigitani na Teresi, wawili kati ya matowashi wa mufalme waliokuwa walinzi wa milango ya vyumba vya mufalme, walikasirika hata wakafanya shauri baya la kumwua mufalme Ahasuero.


Mordekayi akapata habari hiyo, akamujulisha malkia Esteri, naye Esteri akamupasha mufalme habari.


Uchunguzi ulipofanywa, iligunduliwa kwamba ni kweli; basi, watu hao wawili wakatundikwa juu ya muti. Habari juu ya tukio hilo iliandikwa katika kitabu cha Mambo ya Siku mbele ya mufalme.


Kama nimepata kukubaliwa mbele yako, ewe mufalme, na ikikupendeza kukubali ombi langu, basi, ninaomba wewe na Hamani mukuje kesho kwenye karamu nyingine nitakayowaandalia. Wakati huo nitakujulisha ombi langu.”


Wamasikini na wakosefu wakitafuta maji lakini hawayapati, wakiwa wamekauka koo kwa kiu, mimi Yawe nitawajibu; mimi Mungu wa Israeli, sitawaacha.


Katika mwaka wa pili wa utawala wake, mufalme Nebukadneza aliota ndoto. Na kwa hiyo roho yake ikahuzunika sana hata hakuweza kupata usingizi.


Jiwe likaletwa na kuwekwa kwenye mulango wa lile pango. Mufalme akapiga muhuri wake mwenyewe na ule wa wakubwa wake, kusudi uamuzi uliotolewa juu ya Danieli usibadilishwe.


Halafu watu wanaomutii Yawe walizungumuza wao kwa wao, naye Yawe akasikia mazungumuzo yao. Mbele yake kukawekwa kitabu ambamo uliandikwa ukumbusho wa wale wanaomutii na kumuheshimu.


Utajiri wa Mungu, hekima na ufahamu wake ni vikubwa kupita kipimo! Hakuna anayeweza kuvumbua kusudi lake wala kuelewa mipango yake!


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις