Esteri 4:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
1 Mordekayi alipojua yote yaliyotukia, akapasua nguo zake, akavaa nguo ya gunia, na kujitia majivu. Kisha, akapita katikati ya muji akilia kwa sauti ya uchungu.
Akakwenda mpaka kwenye mulango wa nyumba ya mufalme, lakini hakuweza kuingia kwa sababu hakuna mutu aliyeruhusiwa kuingia katika nyumba ya kifalme akiwa amevaa nguo ya gunia.
Katika kila jimbo, mara tu amri ya mufalme ilipotangazwa, kilio kikubwa kiliwapata Wayuda. Wakafunga, wakalia na kuomboleza; na wengi wao wakalala katika majivu wakiwa wamevaa magunia.
Ndiyo maana ninawaambia ninyi: musijali chochote juu yangu, muniache nilie machozi ya uchungu. Musijisumbue kunifariji kwa ajili ya kuangamizwa kwa watu wangu.
Aliwaamuru Eliakimu, musimamizi wa nyumba ya kifalme, Sebuna, katibu, na wazee wa makuhani, wamwendee nabii Isaya mwana wa Amozi, wakiwa wamevaa nguo za magunia.
Munapofunga kula, ninyi munajitaabisha; munaviinamisha vichwa vyenu kama utete, na kulalia nguo za magunia na majivu. Hii ndio munayoita mafungo ya kula chakula? Hiyo ni siku inayonipendeza mimi?
“Ole kwako, muji Korazini! Ole kwako, muji Betesaida! Kwa maana miujiza iliyofanyika ndani yenu ingalifanyika katika muji wa Tiro na muji wa Sidona, wakaaji wa kule wangekwisha zamani kuvaa magunia na kujipakaa majivu, kwa kuonyesha kwamba wamegeuka toka zambi zao.
Nami nitawatuma washuhuda wangu wawili, wakiwa wamevaa nguo za kilio. Nao watatangaza ujumbe wa Mungu kwa muda wa siku elfu moja mia mbili na makumi sita.”