Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Esteri 4:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Mordekayi alipojua yote yaliyotukia, akapasua nguo zake, akavaa nguo ya gunia, na kujitia majivu. Kisha, akapita katikati ya muji akilia kwa sauti ya uchungu.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Esteri 4:1
27 Σταυροειδείς Αναφορές  

Esau aliposikia maneno ya baba yake, akalia kilio kikubwa na cha uchungu. Kisha akamwambia baba yake: “Ee baba yangu, unibariki mimi, tafazali!”


Halafu Yakobo akararua nguo zake kwa huzuni, akavaa nguo ya gunia katika kiuno. Akamulilia mwana wake kwa muda wa siku nyingi.


Daudi akapasua nguo yake kwa huzuni. Hata watu waliokuwa pamoja na Daudi wakafanya vilevile.


Basi, Tamari alijipakaa majivu kwenye kichwa, akapasua kanzu yake, akaweka mikono yake juu ya kichwa, halafu akaondoka akiwa analia kwa sauti.


Akakwenda mpaka kwenye mulango wa nyumba ya mufalme, lakini hakuweza kuingia kwa sababu hakuna mutu aliyeruhusiwa kuingia katika nyumba ya kifalme akiwa amevaa nguo ya gunia.


Katika kila jimbo, mara tu amri ya mufalme ilipotangazwa, kilio kikubwa kiliwapata Wayuda. Wakafunga, wakalia na kuomboleza; na wengi wao wakalala katika majivu wakiwa wamevaa magunia.


Kisha Yobu akasimama, akapasua nguo yake, akanyoa nywele zake, akajitupa chini na kumwabudu Mungu,


Yobu akatwaa kigae, akajikuna nacho na kuikaa kwenye majivu.


Kwa hiyo ninatubu na kujihukumu; ninajinyenyekeza na kuikaa juu ya mavumbi na majivu.


Watu wa Hesiboni na Eleale wanalia, sauti zao zinasikilika mpaka Yasa. Hata waaskari wa Moabu wanalia kwa sauti; mioyo yao inatetemeka.


Ndiyo maana ninawaambia ninyi: musijali chochote juu yangu, muniache nilie machozi ya uchungu. Musijisumbue kunifariji kwa ajili ya kuangamizwa kwa watu wangu.


Mufalme Hezekia aliposikia habari hiyo, alipasua nguo yake, akavaa nguo ya gunia, akaingia katika nyumba ya Yawe.


Aliwaamuru Eliakimu, musimamizi wa nyumba ya kifalme, Sebuna, katibu, na wazee wa makuhani, wamwendee nabii Isaya mwana wa Amozi, wakiwa wamevaa nguo za magunia.


Munapofunga kula, ninyi munajitaabisha; munaviinamisha vichwa vyenu kama utete, na kulalia nguo za magunia na majivu. Hii ndio munayoita mafungo ya kula chakula? Hiyo ni siku inayonipendeza mimi?


Nawe mwanadamu, ujikunje kama mutu aliyekata tamaa, uomboleze mbele yao.


Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:


Nilimwomba Yawe, kwa moyo, nikimutolea maombi pamoja na kufunga kula chakula, nikavaa gunia na kuikaa kwenye majivu.


Kwa sababu hiyo, mimi nitalia na kuomboleza; nitatembea uchi na bila viatu. Nitaomboleza na kulia kama mbweha, nitasikitika na kulia kama mbuni.


Ile siku kubwa ya Yawe imekaribia, iko karibu na inakuja mbio. Mulio wa siku ya Yawe ni wa uchungu; hapo, hata shujaa atalia kwa sauti.


“Ole kwako, muji Korazini! Ole kwako, muji Betesaida! Kwa maana miujiza iliyofanyika ndani yenu ingalifanyika katika muji wa Tiro na muji wa Sidona, wakaaji wa kule wangekwisha zamani kuvaa magunia na kujipakaa majivu, kwa kuonyesha kwamba wamegeuka toka zambi zao.


Lakini Barnaba na Paulo waliposikia habari ile, wakapasua nguo zao kwa huzuni, wakaingia haraka katikati ya kundi la watu, na kusema kwa sauti:


Yoshua akapasua nguo yake, yeye pamoja na wazee wa Israeli. Wakajitupa chini ya Sanduku la Yawe mpaka magaribi; wakajitia mavumbi juu ya vichwa vyao.


Nami nitawatuma washuhuda wangu wawili, wakiwa wamevaa nguo za kilio. Nao watatangaza ujumbe wa Mungu kwa muda wa siku elfu moja mia mbili na makumi sita.”


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις