Esteri 3:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20024 Kila siku walimushauria aache tabia hiyo, lakini Mordekayi hakukubaliana nao. Alikataa kufanya hivyo akisema kwamba yeye ni Muyuda na kwa hiyo hawezi kuinama mbele ya Hamani. Basi, wakamujulisha Hamani kusudi waone kama ataivumilia tabia ya Mordekayi. Δείτε το κεφάλαιο |
Basi, walikwenda kwa mufalme na kumushitaki Danieli kwa kutumia ile sheria, wakisema: Mufalme Dario, haukutia sahihi kwenye sheria kwamba kwa muda wa siku makumi tatu hakuna mutu yeyote atakayeruhusiwa kuomba kitu chochote, kwa mungu yeyote, au kwa mutu yeyote isipokuwa kutoka kwako wewe, ee mufalme, na kwamba yeyote atakayevunja sheria hii atatumbukizwa katika pango la simba? Mufalme akaitikia: Hivi ndivyo inavyokuwa kulingana na sheria ya Wamedi na Wapersi ambayo haiwezi kuvunjika.