Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Esteri 3:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Kila siku walimushauria aache tabia hiyo, lakini Mordekayi hakukubaliana nao. Alikataa kufanya hivyo akisema kwamba yeye ni Muyuda na kwa hiyo hawezi kuinama mbele ya Hamani. Basi, wakamujulisha Hamani kusudi waone kama ataivumilia tabia ya Mordekayi.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Esteri 3:4
11 Σταυροειδείς Αναφορές  

Yule mwanamuke akaendelea kumushawishi Yosefu siku kwa siku, lakini Yosefu hakumusikiliza wala kukubali kulala naye.


Basi sasa, kila mutu kati yenu ninyi wote munaokuwa watu wake, Mungu wake akuwe naye na aende katika Yerusalema huko Yuda, na kuijenga upya nyumba ya Yawe, Mungu wa Israeli, Mungu anayeabudiwa kule Yerusalema.


Wakubwa mbalimbali wa mufalme waliokuwa kwenye mulango wa mufalme, wakamwuliza Mordekayi: “Mbona wewe unaizarau amri ya mufalme?”


Hamani akawaka hasira alipojua kwamba Mordekayi hainami wala kupiga magoti mbele yake.


Sasa, kuna Wayuda fulani uliowachagua kwa kushugulikia mambo ya utawala wa jimbo la Babeli, nao ni: Sadiraki, Mesaki na Abedenego; watu hawa, ee mufalme, hawakutii amri yako. Wanakataa kuitumikia miungu yako na kuiabudu ile sanamu ya zahabu uliyoisimamisha.


Basi, walikwenda kwa mufalme na kumushitaki Danieli kwa kutumia ile sheria, wakisema: Mufalme Dario, haukutia sahihi kwenye sheria kwamba kwa muda wa siku makumi tatu hakuna mutu yeyote atakayeruhusiwa kuomba kitu chochote, kwa mungu yeyote, au kwa mutu yeyote isipokuwa kutoka kwako wewe, ee mufalme, na kwamba yeyote atakayevunja sheria hii atatumbukizwa katika pango la simba? Mufalme akaitikia: Hivi ndivyo inavyokuwa kulingana na sheria ya Wamedi na Wapersi ambayo haiwezi kuvunjika.


Yona akawajibu: Mimi ni Mwebrania; ninamwabudu Yawe, Mungu wa mbingu, muumba wa bahari na inchi kavu.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις