Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Esteri 1:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Lakini Vashiti akakataa kufika kwa amri mufalme aliyotoa kwa njia ya matowashi. Kwa hiyo, mufalme akakasirika sana na hasira yake ikawaka.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Esteri 1:12
19 Σταυροειδείς Αναφορές  

Kisha akamwambia mwanamuke: “Nitakuzidishia uchungu wa kuzaa, Utazaa watoto kwa uchungu. Utakuwa na hamu na mume wako, naye atakutawala.”


Akawaamuru hao wamuletee malkia Vashiti, akiwa amevaa taji yake ya kimalkia. Malkia yule alikuwa na sura nzuri sana, hivyo mufalme alitaka kuwaonyesha wageni wake na viongozi uzuri wake.


Ilikuwa desturi ya mufalme kupata mashauri kutoka kwa wenye hekima, hivyo akawaita wanasheria na waamuzi kusudi wamushaurie la kufanya.


Mufalme akasimama kwa hasira, akatoka ndani ya chumba kwenye karamu ya divai na kwenda inje kwenye bustani ya nyumba ya kifalme. Hamani alipoona kwamba mufalme amekusudia kumwazibu, akabaki nyuma kwa kumusihi malkia Esteri ayaponyeshe maisha yake.


Mashairi ya Asafu. Kwa nini, ee Mungu, umetutupilia kabisa? Mbona hasira yako inawaka juu ya kondoo wako?


Ee Yawe, utakasirika hata milele? Hasira yako itawaka kama moto hata wakati gani?


Mara tu walipokaribia kambi walimwona yule mwana-ngombe na watu wakicheza. Hapo hasira ya Musa ikawaka kama moto, akatupa chini vile vibao kutoka mikono yake na kuvivunja pale chini ya mulima.


Haruni akamujibu: Ninakuomba, ee bwana wangu, hasira yako isiniwakie mimi mutumishi wako. Unafahamu jinsi watu hawa wanavyokuwa tayari kutenda maovu.


Kasirani ya mufalme ni kama ngurumo ya simba, lakini upendo wake ni kama umande juu ya majani.


Kasirani kali ya mufalme ni kama simba anayenguruma; anayemukasirikisha anahatarisha maisha yake.


Kusikia hivyo, mufalme Nebukadneza alikasirika na kuwa na hasira sana, akaamuru wenye hekima wote wa Babeli waangamizwe.


Halafu mufalme Nebukadneza, akakasirika, akaamuru Sadiraki, Mesaki na Abedenego waletwe mbele yake. Nao wakawaleta mbele ya mufalme.


Kwa hiyo, mufalme Nebukadneza akawaka hasira, sura yake ikabadilika kwa chuki juu ya Sadiraki, Mesaki na Abedenego. Akaamuru kwamba moto wa furu uongezwe mara saba kuliko kawaida yake.


Nani anayeweza kusimama mbele ya kasirani ya Yawe? Nani anayeweza kuvumilia ukali wa hasira yake? Yeye anaimwanga hasira yake inayowaka kama moto, hata mawe makubwa anayapasua vipandevipande.


Wake wawatii waume wao kama vile wanavyomutii Bwana.


Wake wanapaswa kutii waume wao katika kila jambo sawa vile kanisa linavyomutii Kristo.


Yawe atamutenga kutoka kati ya makabila yote ya Israeli apatwe na hasara kufuatana na laana zote za agano zilizoandikwa katika kitabu hiki.


Ninyi wake, muwatii waume wenu, kusudi kukiwa wamoja kati yao wasioamini neno la Mungu, mupate kuwavuta kwa kulisadiki kwa mwenendo wenu muzuri pasipo kuwaambia neno.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις