Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Danieli 2:35 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

35 Mara moja chuma, udongo wa mufinyanzi, shaba, feza na zahabu, vyote vikavunjika vipandevipande na vikakuwa kama maganda kwenye nafasi ya kupepetea ngano wakati wa jua. Upepo ukavipeperushia mbali wala hakukubakia hata kipande kimoja. Lakini lile jiwe lililoivunja ile sanamu likageuka kuwa mulima mukubwa na kuijaza dunia yote.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Danieli 2:35
28 Σταυροειδείς Αναφορές  

Wakati wa kipwa inatoweka, wakati wa jua kali inakauka.


upepo unapovuma juu yake yanatoweka, na mahali yalipokuwa hapaonekani tena.


Wamasikini watakula na kushiba; wanaomutafuta Yawe watamusifu. Mungu awajalie waishi milele!


Bado kidogo, mwovu atatoweka; utamutafuta pale alipokuwa, wala hautamwona.


Kisha nikapita pale, naye hakukuwa tena; nikamutafuta, lakini hakuonekana tena.


Mukuje muone matendo ya Yawe. Muone maajabu aliyofanya katika dunia.


Dunia yote inakuabudu; watu wote wanakuimbia sifa!”


Mataifa yote uliyoumba, yatakuja kukuabudu, ee Bwana; yatatangaza ukubwa wa jina lako.


Katika mulima mutakatifu wa Mungu hakutakuwa ubaya wala uharibifu. Maana kumujua Yawe kutaenea pote katika inchi, kama vile maji yanavyojaa katika bahari.


Muungane, enyi watu wa mataifa, na kufezeheshwa! Musikilize, enyi inchi za mbali katika dunia! Mujiweke tayari na kufezeheshwa. Mujiweke tayari na kufezeheshwa.


Wakati wa wafalme wale, Mungu wa mbinguni ataanzisha ufalme ambao hautaangamizwa hata kidogo. Watu wengine hawataushinda na kuutawala ufalme huo, lakini ufalme huo utaziponda na kuzikomesha falme zilizotangulia, nao utadumu milele.


Basi, watatoweka kama ukungu wa asubui, kama umande unaotoweka upesi; kama makapi yanayopeperushwa kwenye nafasi ya kupepetea, kama moshi unaotoka katika munara wa kutoshea moshi inje.


Yawe anasema: Enyi watu wa Sayuni, musimame muwakanyagekanyage! Nitawapatia nguvu kama ngombe dume mwenye pembe za chuma na kwato za shaba. Mutawasaga watu wa mataifa mengi; mutanitolea mimi mapato yao, mutanitolea mali zao mimi Bwana wa dunia yote.


Siku hiyo nitaufanya Yerusalema kuwa kama jiwe zito kwa watu wote: yeyote atakayelinyanyua atajiumiza mwenyewe. Watu wa mataifa yote katika dunia wataushambulia muji ule.


Kwa maana Kristo anapaswa kutawala mpaka atakapowashinda waadui zake wote na kuwaweka chini ya miguu yake.


Kisha malaika wa saba akapiga baragumu. Halafu sauti kubwa zikasikilika katika mbingu, zikisema: “Sasa utawala juu ya dunia ni wa Bwana wetu na wa Masiya wake. Naye atatawala kwa milele na milele!”


lakini akashindwa na haikuwezekana tena kwake kukaa mbinguni pamoja na wamalaika zake.


Kisha nikaona kiti kikubwa cheupe cha kifalme pamoja na yule aliyeikaa juu yake. Dunia na mbingu vikatoweka mbele yake navyo havikuonekana tena.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις