Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Amosi 7:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Bwana wetu Yawe alinionyesha tena maono mengine: Bwana wetu Yawe akiuita moto wa hukumu wa kuwaazibu watu. Moto ule uliunguza vilindi vikubwa vya bahari, ukaanza kuiteketeza inchi kavu.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Amosi 7:4
22 Σταυροειδείς Αναφορές  

Silikasirikii tena shamba hili; kama miiba na michongoma ingelilishambulia, mimi ningepambana nayo na kuichoma kwa moto.


Enyi jamaa ya Daudi, Yawe anasema hivi: Kila asubui muamue maneno kufuatana na sheria yangu, muwakomboe wote walionyanganywa mali zao toka katika mikono ya watesaji. Kama si vile, hasira yangu itawaka kama moto, wala hakuna atakayeweza kuizimisha, kwa sababu ya matendo yenu maovu.


Enyi watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema, mujitahiri, mukiondoa govi za mioyo yenu, mupate kujitoa kwa Yawe. Kama si vile, kasirani yangu itawaka kama moto, nayo itaunguza wala hakuna atakayeizimisha, kwa sababu ya matendo yenu maovu.


Uwaambie wasikilize neno la Yawe. Uwaambie kwamba Bwana wao Yawe anasema hivi: Nitawasha moto kwako, nao utateketeza miti yote, mibichi na yenye kukauka; utaenea tangu kusini mpaka kaskazini wala hakuna atakayeweza kuzimisha ndimi zake. Nao utaunguza watu wote.


Ninakulilia wewe, ee Yawe, moto umemaliza malisho katika mbuga, ndimi za moto zimeteketeza miti katika mashamba.


Basi, moto ukatokea mbele ya Yawe, ukawateketeza hao vijana, wakakufa mbele yake.


Basi, nitashusha moto juu ya nyumba ya mufalme Hazaeli, na kuziteketeza kabisa nyumba nzuri za mufalme Beni-Hadadi.


Basi, nitashusha moto juu ya kuta za muji wa Gaza, na kuziteketeza kabisa nyumba zake nzuri.


Basi, nitashusha moto juu ya inchi ya Yuda, na kuziteketeza kabisa nyumba nzuri za Yerusalema.


Niliwaangusha wamoja kati yenu kwa maangamizi kama nilivyoangamiza Sodoma na Gomora. Wale waliobaki kati yenu, walikuwa kama kijiti kilichookolewa katika moto. Hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Mutafute Yawe, nanyi mutaishi! Kama sivyo, atawatokea wazao wa Yosefu kama moto; moto utawateketeza wakaaji wa Beteli na hakuna mutu atakayeweza kuuzimisha.


Bwana wetu Yawe alinionyesha hivi: Yawe alikuwa anaumba nzige kundi zima, nyuma ya watu kumaliza kukata majani kwa ajili ya nyama wa mufalme. Wakati ule, majani yalikuwa ndio yanaanza kuchipuka tena.


Yawe alinionyesha tena maono mengine: Yawe alikuwa anasimama karibu na ukuta, akishika katika mukono wake uzi wenye timazi.


Milima itayeyuka chini ya miguu yake, kama inta karibu na moto; mabonde yatapasuka, kama vile maji yanayoporomoka kwenye muteremuko.


Nani anayeweza kusimama mbele ya kasirani ya Yawe? Nani anayeweza kuvumilia ukali wa hasira yake? Yeye anaimwanga hasira yake inayowaka kama moto, hata mawe makubwa anayapasua vipandevipande.


Kisha Yawe akashusha moto ukawateketeza wale watu mia mbili makumi tano waliokwenda kufukiza ubani.


Hasira yangu imewaka moto, inachoma mpaka chini kuzimu, itateketeza dunia na vinavyokuwa ndani yake, itaunguza misingi ya milima.


Lakini juu ya wamalaika, Mungu alisema: “Mungu anawafanya wamalaika wake kuwa kama upepo. Anawafanya hao watumishi wake kuwa kama ndimi za moto.”


Nyuma ya mambo hayo nilipata maono mengine. Niliona mulango mumoja umefunguliwa wazi mbinguni. Halafu ile sauti niliyosikia mara ya kwanza, iliyolia kama baragumu, ikaniambia: “Panda huku, nami nitakuonyesha mambo yanayopaswa kutokea nyuma ya hayo ya mbele.”


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις