Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Amosi 7:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Amosi akamujibu Amazia: Mimi si nabii wa mushahara, wala si mumoja wa kikundi cha manabii. Mimi ni muchungaji na mulimaji wa miti ya mikuyu.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Amosi 7:14
17 Σταυροειδείς Αναφορές  

Haya ni maneno ya Amosi, mumoja wa wachungaji wa nyama wa muji wa Tekoa. Mungu alimufunulia Amosi mambo haya yote juu ya inchi ya Israeli miaka miwili mbele ya tetemeko la inchi, wakati Uzia alipokuwa mufalme wa Yuda, na Yeroboamu mwana wa Yoasi alipokuwa mufalme wa Israeli.


lakini kila mumoja atasema: “Mimi si nabii. Mimi ni mulimaji tu; nimerizi mashamba tangu ujana wangu.”


Elisha akarudi Gilgali wakati katika inchi kulikuwa njaa. Siku moja, alipokuwa akifundisha wanafunzi wa manabii alimwambia mutumishi wake: “Weka chungu kikubwa juu ya moto, uwapikie manabii chakula.”


Wanafunzi wa manabii wa Yeriko wakamwendea Elisha, wakamwuliza: “Unajua kwamba leo Yawe atamupeleka bwana wako?” Elisha akawajibu: “Ndiyo. Ninajua. Munyamaze.”


Lakini nabii Yehu mwana wa Hanani, akakwenda kukutana na mufalme, akamwambia: “Unazani ni vema kuwasaidia waovu na kuwapenda wanaomuchukia Yawe? Mambo uliyofanya yamekuletea kasirani ya Yawe.


Wanafunzi wa manabii wa Beteli wakamwendea Elisha, wakamwuliza: “Unajua kwamba leo Yawe atamupeleka bwana wako?” Elisha akajibu: “Ndiyo. Ninajua. Munyamaze.”


Lakini Mungu anachagua vitu ambavyo watu wanahesabu kuwa vya upumbafu kusudi apatishe wenye hekima haya, naye amechagua vitu wanavyohesabu kuwa vya uzaifu kusudi apatishe wenye nguvu haya.


Matendo mengine ya Yosafati, kutoka mwanzo wa utawala wake mpaka mwisho, yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Yehu mwana wa Hanani, ambacho kiko katika Kitabu cha Wafalme wa Israeli.


Kwa wakati ule, nabii Hanani akamwendea mufalme Asa wa Yuda, akamwambia: “Kwa sababu ulimutegemea mufalme wa Suria kuliko kumutegemea Yawe, Mungu wako, jeshi la mufalme wa Suria limekuponyoka.


Siku moja, wanafunzi wa manabii walimulalamikia Elisha wakisema: “Pahali hapa tunapokaa ni padogo sana kwetu!


Manabii makumi tano wakawafuata mpaka kwenye muto Yordani. Elia na Elisha wakasimama karibu na muto, nao manabii wakasimama mbali kidogo.


Kwa amri ya Yawe, mumoja wa wanafunzi wa manabii akamwambia mwenzake: “Unipige, tafazali.” Lakini mwenzake akakataa kumupiga.


Watu waliomufahamu Saulo zamani, walipomwona anatabiri, wakaulizana: “Kitu gani kimemupata mwana wa Kisi? Hata Saulo ni mumoja wa manabii?”


Elia akaondoka, akamukuta Elisha mwana wa Safati akilima. Pale, kulikuwa makundi kumi na mbili ya ngombe dume wawiliwawili wakilima, na ngombe wawili wa Elisha walikuwa wa nyuma kabisa. Basi, Elia akavua koti lake na kumutupia.


Wale wanafunzi wa manabii kutoka Yeriko walipomwona, walisema: “Roho wa Elia yuko kwa Elisha.” Basi, wakaenda kumupokea, wakainama mbele yake kwa heshima.


Walichuma mimea katika jangwa na majani katika pori wakakula, walikula hata mizizi ya muti wa vifagio.


Simba akinguruma, ni nani asiyeogopa? Bwana wetu Yawe akisema, ni nani atakataa kuutangaza ujumbe wake?


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις