Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Amosi 6:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Muende Kalne, muangalie. Tokea kule muende mpaka katika ule muji mukubwa wa Hamati, kisha mutelemuke mpaka Gati kwa Wafilistini. Mutatambua kwamba ninyi si bora kuliko falme zile, hata kama eneo lao ni ndogo zaidi ya lenu.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Amosi 6:2
19 Σταυροειδείς Αναφορές  

Miji ya kwanza ya utawala wake ilikuwa Babeli, Ereki, na Akadi katika inchi ya Sinari.


Wakati Toi, mufalme wa Hamati, aliposikia kwamba Daudi amewashinda waaskari wote wa Hadadezeri,


Naye Solomono kwa muda wa siku saba alifanya sikukuu pamoja na Waisraeli wote. Nao walitoka tangu kwenye kiingilio cha Hamati, mpaka muto wa Misri.


Kisha mufalme wa Asuria akapeleka watu kutoka Babeli, Kuta, Awa, Hamati na Sefarwaimu na kuwaweka katika miji ya Samaria kwa pahali pa watu wa Israeli waliopelekwa katika uhamisho. Wakaitwaa miji hiyo na kukaa mule.


Watu wa Babeli walitengeneza sanamu za Sukoti-Benoti, watu wa Kuta wakatengeneza sanamu za Nergali, watu wa Hamati sanamu za Asima,


Iko wapi ile miungu ya Hamati na Arpadi? Iko wapi ile miungu ya Sefarwaimu, Hena na Iwa? Imeokoa Samaria toka katika mikono yangu?


Wako wapi wafalme wa Hamati, Arpadi, Sefarwaimu, Hena na Iwa?’ ”


Uzia akaondoka kwa kupigana vita na Wafilistini, akabomoa kuta za miji ya Gati, Yabune na Asidodi. Akajenga miji katika eneo la Asidodi na fasi ingine katika inchi ya Filistia.


Hii ni juu ya Damasiki: Miji ya Hamati na Arpadi, imejaa wasiwasi kwa kufikiwa na habari mbaya; mioyo ya watu wake inayeyuka kwa hofu, imefazaika kama bahari isiyoweza kutulia.


Wewe Ninawe, ni bora kuliko Tebe, muji uliojengwa pembeni ya muto Nili? Tebe ulizungukwa na maji, bahari ilikuwa kikingio chake, maji yalikuwa ukuta wake!


Alipokuwa anaongea nao, Goliati, yule shujaa wa Wafilistini kutoka Gati, alijitokeza mbele ya waaskari wa Israeli kama vile alivyozoea. Naye Daudi alimusikiliza vizuri sana.


Kutoka kwenye kambi ya Wafilistini, shujaa mumoja anayeitwa Goliati, wa muji wa Gati, alijitokeza. Urefu wake ulikuwa metre tatu.


Hivyo, wakalipeleka Sanduku hilo la Mungu kwenye muji wa Ekuroni. Lakini Sanduku hilo la Mungu lilipofika kule, watu wa muji huo walipiga kelele: “Wametuletea Sanduku la Mungu wa Israeli kwa kutuua sisi na watu wetu.”


Walituma wajumbe na kuwakusanya wakubwa wote wa Wafilistini na kuwauliza: “Tutafanya nini na Sanduku hili la Mungu wa Israeli?” Wakubwa wao wakajibu: “Sanduku hilo la Mungu wa Israeli mulipeleke Gati.” Basi, wakalipeleka kwenye muji wa Gati.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις