Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Amosi 5:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Huyo aliyezifanya nyota zinazoitwa Kilimia na Orioni, ambaye analigeuza giza nene kuwa muchana, na muchana kuwa usiku; yeye anayekusanya maji ya bahari na kuyamwanga juu ya inchi kavu, Yawe ndilo jina lake.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Amosi 5:8
23 Σταυροειδείς Αναφορές  

Anafunua vilindi vya giza, na kuleta katika mwangaza mambo yaliyokuwa katika giza.


Mungu anatimiza mapenzi yake katika dunia, ikuwe ni kwa ajili ya kuwaazibu watu, au kwa ajili ya kuonyesha wema wake.


Unaweza kupiga vigelegele na kuyaamuru mawingu yakufunike kwa mutiririko wa mvua?


Yeye aliweka makundi ya nyota katika anga: Dubu, Orioni, Kilimia, na Vyumba vya Kusini.


Unaleta giza, nao usiku unaingia; nao wanyama wote wa pori wanatoka:


Mungu akaleta giza juu ya inchi; lakini Wamisri wakakataa kutii amri zake.


Nitawaongoza vipofu katika njia wasiyoifahamu, nitawaongoza katika njia ambazo hawazijui. Mbele yao nitaligeuza giza kuwa mwangaza, na pahali penye kuharibika patakuwa laini. Huo ndio mupango wangu wa kufanya, nami nitautimiza.


Kama vipofu tunapapasapapasa ukuta; tunasitasita kama watu wasiokuwa na macho. Tunajikwaa muchana kati, sawa vile ni usiku; kati ya wenye afya, sisi ni kama wafu.


Kwa hiyo, Yawe anasema: Wakati huu nitawafundisha kusudi wapate kutambua waziwazi nguvu zangu na uwezo wangu, nao watajua kwamba jina langu ni Yawe.


Yawe aliyeiumba dunia, Yawe aliyeifanya na kuiimarisha dunia, yule ambaye jina lake ni Yawe, anasema hivi:


Mungu ndiye aliyeifanya milima, na kuumba upepo; ndiye anayemujulisha mwanadamu mawazo yake; ndiye anayegeuza muchana kuwa usiku, na kukanyaga vilele vya dunia. Yawe wa majeshi ndilo jina lake!


Siku hiyo, nitalifanya jua litue pa saa sita za muchana, na kuijaza inchi giza wakati wa muchana. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Yawe amejenga makao yake mbinguni, nayo dunia akaifunika kwa anga; anayaita maji ya bahari, na kuyamwanga juu ya inchi kavu. Yawe, ndilo jina lake!


Watu hao wanaokaa katika giza, mwangaza umewatokea! Hao wanaoishi katika inchi yenye giza nzito sana ya lufu, wameona mwangaza mukubwa.”


Atawaangazia wale wanaoishi katika giza na wanaokaa katika kivuli cha kifo, kusudi atuongoze tupate kufuata njia ya amani.”


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις