Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Amosi 5:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Lakini musinitafutie kule Beteli wala musiende Gilgali wala musivuke kwenda Beri-Seba. Maana wakaaji wa Gilgali, hakika watapelekwa katika uhamisho, na Beteli utaangamizwa!

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Amosi 5:5
34 Σταυροειδείς Αναφορές  

Kwa hiyo kisima hicho kikaitwa Beri-Seba, maana wote wawili walifanya kiapo pahali pale.


Abrahamu akapanda muti wa mukwaju kule Beri-Seba, akaomba kwa jina la Yawe, akamwabudu Mungu, Mungu wa milele.


Kutoka kule, Isaka alikwenda Beri-Seba.


Basi, Isaka akakiita kisima hicho Siba, ni kusema “Kiapo”. Kwa hiyo jina la muji ule ni Beri-Seba hata leo.


Basi, kisha kushauriana na wengine, akatengeneza sanamu mbili za zahabu. Kisha akawaambia watu: “Enyi watu wa Israeli, hii ndiyo miungu yenu iliyowatoa katika inchi ya Misri! Hakuna sababu ya kwenda Yerusalema kutoa sadaka kule.”


Akaiweka sanamu moja katika muji wa Beteli, na ya pili katika muji wa Dani.


Akakusanya makuhani wote kutoka miji ya Yuda na aliharibu pahali pa kuabudia makuhani walipofukiza ubani, kutoka Geba mpaka Beri-Seba. Akabomoa pahali pa kuabudia palipokuwa upande wa kushoto wa mulango wa muji kwenye milango iliyokuwa kwenye njia ya kuingilia kwenye mulango wa Yoshua mutawala wa muji.


Wale wanaokuchukia watapata haya, makao ya waovu yatatoweka kabisa.


Yawe anavunja mipango ya mataifa, na anabadilisha mawazo yao.


Watesaji watatoweka, wenye kumuchekelea Mungu watakwisha, wote wanaokusudia kutenda maovu watateketezwa.


Mushauriane pamoja lakini itakuwa bure; mufanye mipango lakini haitawezekana, maana Mungu Yuko Pamoja Nasi.


Halafu Wamoabu watapata haya kwa ajili ya mungu wao Kemosi, kama vile watu wa Israeli walivyopata haya kwa ajili ya kutegemea Beteli.


Pahali pa kutambikia juu ya vilima pa Aweni, pahali Waisraeli walipofanyia zambi, pataharibiwa. Miiba na michongoma vitaota katika mazabahu zao. Nao wataiambia milima: Mutufunike na vilima: Mutuangukie!


Mimi niliongea na manabii; ni mimi niliyewapa maono mengi, na kwa njia yao nilitangaza mupango wangu.


Ikiwa kweli ninyi Waisraeli ni wazinzi lakini, watu wa Yuda basi wasianguke ndani ya makosa! Musiende pahali patakatifu kule Gilgali, wala musiende kule Nyumba ya Uovu. Wala musiape mukisema: Kama vile Yawe anavyoishi!


Yawe anasema hivi: Uovu wao wote ulianzia Gilgali; kule ndiko nilipoanza kuwachukia. Kwa sababu ya uovu wa matendo yao, nitawafukuza toka katika nyumba yangu. Sitawapenda tena. Wakubwa wao wote ni waasi.


Nitavivunjavunja vifungio vya milango ya muji wa Damasiki, na kuwaondoa wakaaji wa bonde la Aweni, pamoja na mutawala wa Beti-Edeni. Waaramu wanapelekwa katika uhamisho kule Kiri. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Siku nitakapowaazibu Waisraeli kwa sababu ya makosa yao, nitayaharibu vilevile mazabahu ya muji wa Beteli. Nitazikata pembe za kila mazabahu na kuziangusha chini.


Enyi Waisraeli, muende basi kule Beteli na kuniasi! Muende Gilgali muongeze makosa yenu! Mutoe sadaka zenu kila asubui na zaka zenu kwa siku ya tatu.


Basi, Amazia kuhani wa muji wa Beteli, akamupelekea mufalme Yeroboamu wa Israeli habari hii: Amosi analeta fitina juu yako katika ufalme wa Israeli. Hotuba zake ni hatari kwa inchi hii.


Usitoe tena unabii hapa katika Beteli, kwa sababu hapa ni pahali ya ibada ya mufalme; ni hekalu la utawala huu.


Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Muke wako atakuwa kahaba katika muji, na wana wako na wabinti zako watauawa katika vita. Inchi yako itagawanywa na kupewa wengine, nawe mwenyewe utakufia katika inchi inayohesabiwa kuwa chafu; nao Waisraeli hakika watapelekwa katika uhamisho, mbali kabisa na inchi yao.


Kule kwenye vilima ambapo wazao wa Isaka wanatambikia, kutafanywa kuwa uharibifu mutupu na mahekalu ya Waisraeli yatakuwa mabomoko. Nitaushambulia kwa vita ukoo wa mufalme Yeroboamu.


Wale wanaoapa kwa mungu wa uongo wa Samaria na kusema “Kwa nafsi ya mungu wako ee Dani” au “Kwa nafsi ya mungu wa Beri-Seba”, wote wataanguka na hawatasimama tena hata kidogo.


Mungu amechagua vitu ambavyo watu wanahesabu kuwa vya hali ya chini na vyenye kuzarauliwa, visivyokuwa na maana mbele ya macho ya watu, kusudi aharibu vile wanavyohesabu kuwa vya lazima.


Ingawa vile, mimi ninatangaza mambo ya hekima kwa watu waliokomaa kiroho. Lakini mambo haya si ya hekima ya kidunia, wala ya watawala wa dunia hii watakaoangamizwa.


Mutazaa watoto wanaume na wanawake, lakini hawatakuwa wenu, watapelekwa katika uhamisho.


Kisha Yawe akamwambia Yoshua: “Leo hii nimewaondolea ile haya ya Misri.” Hivyo pahali pale pakaitwa Gilgali mpaka hivi leo.


Kwa muda wa saa moja tu utajiri mwingi kama huu umeharibishwa.” Waongozi wote wa mashua na wasafiri wao, nao wote wanaofanya kazi ndani ya mashua na wote wanaochuuza kwa njia ya bahari walisimama kwa mbali.


Samweli akawaambia: “Twende wote Gilgali na kwa mara ingine tutamutangaza Saulo kuwa mufalme.”


Kila mwaka Samweli alitembelea Beteli, Gilgali na Misipa, na kuwaamulia Waisraeli haki zao katika miji hiyo yote.


Mwana wake wa kwanza aliitwa Yoeli, na wa pili aliitwa Abiya. Wote wawili walikuwa waamuzi kule Beri-Seba.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις