Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Amosi 3:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Waadui wataizunguka inchi yenu, wataharibu kuta zako, na kuziteka nyumba zao nzuri.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Amosi 3:11
17 Σταυροειδείς Αναφορές  

Enyi Waisraeli, kweli nitaleta taifa moja likuje kuwashambulia. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nalo litawatesa ninyi kuanzia Hamati upande wa kaskazini, mpaka kwenye kijito cha Araba, upande wa kusini.


Basi, nitashusha moto juu ya inchi ya Yuda, na kuziteketeza kabisa nyumba nzuri za Yerusalema.


Bwana wetu Yawe ameapa kwa nafsi yake: Ninachukizwa sana na kiburi cha wazao wa Yakobo; tena ninachukia nyumba zao nzuri sana. –Ni ujumbe wa Yawe.– Muji wao na vyote vinavyokuwa ndani yake nitavipatia waadui zake.


Nitaziharibu nyumba zote katika muji na katika vijiji; nitazibomoa nyumba zilizopambwa kwa pembe za tembo, nyumba kubwakubwa zitaanguka. –Ni ujumbe wa Yawe.


Hawajui kabisa kutenda mambo yanayokuwa sawa! –Ni ujumbe wa Yawe.– Wamejaza nyumba zao nzuri na vitu vya wizi na mateso.


Aliichoma moto nyumba ya Mungu, akaubomoa ukuta wa Yerusalema, akazichoma moto nyumba zote za kifalme na kuharibu vyombo vyake vyote vya bei kali.


Wakati wa utawala wa Peka mufalme wa Israeli, Tigilati-Pileseri, mufalme wa Asuria, aliteka miji ya Iyoni, Abeli-Beti-Maka, Yanoa, Kadesi na Hazori, pamoja na inchi za Gileadi, Galilaya na Nafutali na kuwahamisha wakaaji wake kwenda Asuria.


Basi, Puli mufalme wa Asuria akashambulia inchi ya Israeli, naye Menahemu akamupa kilo elfu makumi tatu na ine za feza kusudi amusaidie kuimarisha mamlaka yake juu ya inchi ya Israeli.


Nyuma ya mauaji hayo, wana wengine wa Yakobo wakaingia katika muji na kunyanganya mali yote katika muji ule, kwa sababu dada yao alikuwa amechafuliwa.


Kisha kula hakuacha hata makombo. Kwa hiyo fanaka yake yote haitadumu.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις