Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Amosi 2:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Niliwatoa ninyi kutoka inchi ya Misri, nikawaongoza kupitia katika jangwa miaka makumi ine, mpaka mukaitwaa inchi ya Waamori kuwa yenu.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Amosi 2:10
26 Σταυροειδείς Αναφορές  

Ukawatunza katika jangwa kwa miaka makumi ine na hawakukosa kitu chochote; nguo zao hazikuchakaa wala miguu yao haikuvimba.


Kwa miaka makumi ine nilichukizwa nao, nikasema: ‘Kweli, hawa ni watu waliopotoka! Hawajali kabisa njia zangu!’


Siku hiyohiyo Yawe aliwatoa Waisraeli katika inchi ya Misri kwa makundi.


Mimi ni Yawe, Mungu wako, niliyekutoa katika inchi ya Misri, ambako ulikuwa mutumwa.


na hivyo, nimeshuka kusudi niwaokoe toka mikono ya Wamisri. Nitawatoa katika inchi na kuwapeleka katika inchi nzuri na kubwa, inchi inayotiririka maziwa na asali, inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.


Hawakujiuliza hivi: Yuko wapi Yawe aliyetuondoa katika inchi ya Misri, aliyetuongoza katika mbuga, katika inchi ya jangwa na mashimo, inchi inayokauka na yenye giza kubwa, inchi isiyopitiwa na mutu yeyote, wala kukaliwa na mwanadamu?


Basi, mimi niliwatoa katika inchi ya Misri, nikawapeleka katika jangwa.


Enyi Waisraeli, musikilize neno Yawe alilosema juu yenu, enyi taifa zima alilolitoa katika inchi ya Misri:


Kwangu mimi, ninyi Waisraeli, muko sawasawa na watu wa Kushi! –Ni ujumbe wa Yawe.– Niliwatoa Wafilistini kutoka Krete, na Waaramu kutoka Kiri, kama nilivyowatoa ninyi kutoka Misri.


Mimi niliwatoa katika inchi ya Misri, niliwakomboa kutoka katika utumwa, niliwapatia Musa, Haruni na Miriamu kwa kuwaongoza.


Kwa hiyo wakaeneza mambo ya uongo kati ya watu wa Israeli juu ya inchi waliyoipeleleza, wakisema: Inchi hiyo inawaua watu wake. Vilevile watu wote tuliowaona huko ni wakubwa sana.


Waisraeli wakaiteka miji hii yote nao wakaishi katika miji ya Waamori katika Hesiboni na vijiji vyake.


Yawe akawaka hasira juu ya Waisraeli, akawafanya watangetange katika jangwa kwa muda wa miaka makumi ine; kizazi kizima kilichokuwa kimefanya maovu mbele yake kikakufa.


na kuwavumilia katika jangwa kwa muda wa miaka makumi ine.


Basi Mungu akajitenga mbali nao, akawaacha waabudu nyota, jua na mwezi kufuatana na maneno haya yaliyoandikwa katika kitabu cha manabii: ‘Ninyi watu wa Israeli, si mimi muliyemuchinjia nyama na kumutolea sadaka zingine kwa muda wa ile miaka makumi ine katika jangwa.


Kisha Yawe akatuambia sisi wote: ‘Hao watoto wenu munaoogopa kwamba watakuwa mateka za waadui zenu, hakika hao wanaokuwa wadogo ambao hawajui bado kupambanua kati ya mazuri na mabaya, hao ndio watakaoingia huko, nami nitawapa wao inchi hiyo ikuwe yao.


“Basi, mukumbuke jinsi Yawe Mungu wenu alivyowabariki ninyi katika kila jambo mulilofanya. Aliwatunza mulipokuwa munatangatanga katika jangwa hili kubwa. Amekuwa pamoja nanyi miaka hii yote makumi ine na hamukupungukiwa na kitu chochote.


upande wa kusini. Vilevile inchi za Wakanana kuanzia Ara ya Wasidoni mpaka Afeki kwa mupaka wa Waamori;


Kisha niliwaongoza mpaka katika inchi ya Waamori ambao waliishi upande mwingine wa muto Yordani. Walipigana nanyi, lakini mimi niliwapa ushindi juu yao mukawaangamiza na kuiteka inchi yao.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις