Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Amosi 1:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Damasiki, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamekatakata watu wa Gileadi wakitumia majembe ya mashini ya kulima.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Amosi 1:3
26 Σταυροειδείς Αναφορές  

Basi, mutu yeyote atakayepona kuuawa kwa upanga wa Hazaeli, Yehu atamwua, na yeyote atakayepona kuuawa kwa upanga wa Yehu, Elisha atamwua.


Yawe alikasirika, akawafanya watu wa Israeli washindwe katika vita mara kwa mara na mufalme Hazaeli wa Aramu na mwana wake Beni-Hadadi.


Yoahazi hakukuwa na waaskari, lakini alikuwa tu na wapanda-farasi makumi tano, magari kumi na waaskari wa miguu elfu kumi. Hii ilikuwa ni kwa sababu mufalme wa Aramu alikuwa ameyaangamiza makundi ya waaskari ya Israeli na kuyakanyaga chini kama mavumbi.


Tigilati-Pileseri, akiitika kwa ombi la Ahazi, aliushambulia muji wa Damasiki na kuuteka. Akamwua mufalme Resini na kuwapeleka wafungwa kule Kiri.


Hazaeli akamwuliza: “Bwana wangu, mbona unalia?” Elisha akamujibu: “Kwa sababu ninajua maovu ambayo utawatendea watu wa Israeli. Utateketeza kuta zao kwa moto, na kuwaua vijana wao, utawapondaponda watoto wao na kupasua wanawake wenye mimba tumbo.”


Mara hizi zote kumi mumenitukana. Basi, hamusikii haya kunitendea vibaya?


Atakuokoa mara sita toka katika magumu; hata mara saba hasara haitakugusa.


Kuna vitu sita Yawe anavyochukia, hata saba ambavyo ni chukizo kwake:


Gawa sehemu moja kwa watu saba hata wanane, maana, haujui hasara itakayofika katika dunia.


Kunde haipepetwi kwa chombo kikali wala mbegu za vikolezo kwa gari! Lakini kunde zinapepetwa kwa fimbo na mbegu za vikolezo kwa kijiti.


Nitawafanya mukuwe kama chombo cha kupepeta, chenye meno mapya na makali. Mutaipepeta milima na kuipondaponda; mutavisagasaga vilima kama maganda.


Maana, mbele mutoto huyo hajajua kukataa mabaya na kuchagua mema, inchi za wafalme hao wawili unaowaogopa zitakuwa ukiwa.


Maana muji mukubwa wa Aramu ni Damasiki, na huyo Resini ni mukubwa wa Damasiki tu. Muji mukubwa wa Efuraimu ni Samaria, na mwana wa Remalia ni mukubwa wa Samaria tu. Katika miaka makumi sita na mitano utawala wa Efuraimu utavunjwa; Efuraimu halitakuwa taifa tena. Kama hautaamini, hautaimarika.


Maana mbele mutoto huyu hajafikia umri wa kuweza kutamka neno “Baba” au “Mama”, utajiri wa muji wa Damasiki na vitu walivyonyanganya kule Samaria vitapelekwa kwa mufalme wa Asuria.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Edomu, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamewawinda wandugu zao Waisraeli kwa mapanga, wakaitupilia mbali huruma yao yote ya kindugu. Hasira yao haikuwa na mwisho, waliiacha iwake siku zote.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Amoni, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Katika vita yao kwa kupanua inchi, walipasua tumbo za wanawake wenye mimba katika inchi ya Gileadi.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Gaza, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamekamata watu wengi na kuwapeleka kwa Waedomu.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Tiro, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamekamata watu wengi na kuwapeleka mpaka Edomu. Hawakutii mapatano ya urafiki waliokuwa wamefanya.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Moabu, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamemukosea heshima marehemu mufalme wa Edomu kwa kuichoma mifupa yake kwa moto kwa kujitengenezea chokaa!


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Yuda, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamezarau sheria zangu, wala hawakufuata masharti yangu. Wamepotoshwa na miungu ileile babu zao waliyoifuata.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya Waisraeli, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wameuzisha watu wa haki kuwa watumwa kwa maana hawakuweza kulipa madeni yao; na kuwauzisha wakosefu wanaoshindwa kulipa deni la muguu mumoja wa mapapa.


Ujumbe wa Yawe: Neno la Yawe ni juu ya azabu ya miji Hadiraki na Damasiki. Maana inchi ya Aramu ni mali ya Yawe, kama vile makabila yote ya Israeli yanavyokuwa,


vilevile muji wa Hamati unaopakana na Hadiraki, na hata miji ya Tiro na Sidona ingawa inajiona kuwa na hekima sana.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις