Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




2 Yoane 1:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Mungu Baba pamoja na Yesu Kristo, Mwana wa Baba, watatujalia neema, huruma na amani katika ukweli na upendo.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




2 Yoane 1:3
9 Σταυροειδείς Αναφορές  

Yawe wa majeshi anasema hivi: Siku za mafungo ya kula chakula ya mwezi wa ine, mwezi wa tano, mwezi wa saba na mwezi wa kumi, zitakuwa nyakati za furaha na shangwe; zitakuwa sikukuu za shangwe kwa watu wa Yuda. Basi, mupende ukweli na amani.


Ninawaandikia ninyi wote wapenzi wa Mungu munaokaa Roma, mulioitwa kuwa watu wake watakatifu. Ninawatakia neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.


Kwa maana kwa wale wanaoungana na Kristo Yesu, kutahiriwa au kutokutahiriwa hakufai kitu. Kitu kinachofaa ni imani inayotenda kazi kwa upendo.


Bwana wetu amenijalia neema kwa uwingi, amenipa imani na upendo tunaokuwa nao katika kuungana kwetu na Kristo Yesu.


Ninakuandikia wewe Timoteo mwana wangu wa kweli katika imani. Ninakutakia neema na rehema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Kristo Yesu Bwana wetu.


Ushike maneno ya kweli niliyokufundisha, yapate kuwa mufano kwako. Ushikamane na imani na upendo unaokuwa nao kwa njia ya kuungana kwako na Kristo Yesu.


Na huu ndio upendo: si kwamba sisi tulimupenda Mungu, lakini kwamba ni yeye ndiye aliyetupenda hata akatuma Mwana wake kama vile sadaka iliyotolewa kwa ajili ya usamehe wa zambi zetu.


Barua hii inatoka kwangu mimi muzee. Ninakuandikia wewe mama uliyechaguliwa na Mungu, pamoja na watoto wako ninaowapenda hakika. Wala si mimi peke tu ninayewapenda, lakini vilevile wale wote wanaojua ule ukweli wanawapenda ninyi,


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις