2 Na sasa katika hali hii tunaugua kwa maana tunatamani sana kuvaa makao yetu yanayotoka mbinguni.
Na si viumbe hivi tu; hata sisi tuliokwisha kuwa na Roho wa Mungu kama sehemu ya kwanza ya zawadi Mungu atakazotoa, tunaugua vilevile ndani yetu, tukingojea kukubaliwa na Mungu kuwa watoto wake, maana yake kukombolewa kwa kimwili.
Maana ninasongwa na mambo mawili. Ninatamani kujiendea na kukaa pamoja na Kristo, maana hili ndilo jambo bora zaidi.
Ole kwangu, mimi mutu wa taabu! Ni nani atakayeniokoa kutoka katika mwili huu unaokuwa wa kufa?
Sasa nitawaambia ninyi siri: sisi wote hatutakufa, lakini sisi wote tutabadilishwa
Uliuumba mwili wangu kwa mifupa na mishipa, ukaifunika mifupa yangu kwa nyama na ngozi.