Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




2 Samweli 4:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Daudi akawaamuru vijana wake, nao wakawaua. Wakawakata mikono na miguu. Halafu wakawatundika juu ya muti pembeni ya kisima kule Hebroni. Lakini walikichukua kichwa cha Isiboseti na kukizika katika kaburi la Abeneri kule Hebroni.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




2 Samweli 4:12
8 Σταυροειδείς Αναφορές  

Kisha, Daudi akamwita mumoja kati ya vijana wake akamwambia: “Umwue mutu huyu!” Yule kijana alimupiga yule Mwamaleki, naye akakufa.


Yawe amekulipiza kisasi kutokana na kumwanga damu ya watu wote wa jamaa ya Saulo, ambaye sasa wewe umenyanganya ufalme kwa pahali pake. Sasa, Yawe amemupa mwana wako Abusaloma ufalme. Maangamizi yamekupata kwa sababu wewe ni mwuaji.”


Abeneri mwana wa Neri, mukubwa wa waaskari wa Saulo alikuwa amemukamata Isiboseti mwana wa Saulo na kumupeleka kule Mahanaimu.


Daudi aliwatoa watoto hao saba wanaume kwa Wagibeoni, nao wakawatundika kwenye mulima mbele ya Yawe, wote saba wakakufa pamoja. Watoto hao waliuawa kwa mwanzo wa mavuno ya Shayiri.


Abeneri alizikwa kule Hebroni na mufalme aliomboleza kwa sauti akiwa pembeni ya kaburi. Watu wengine wote walifanya vile vile.


Utue muzigo wako kwa Yawe, naye atakusaidia; hamwachilii mutu wa haki ashindwe.


Kwa maana mutahukumiwa kufuatana na namna munavyowahukumu wengine, na kipimo kile munachowapimia wengine ndicho kitakachotumiwa kwenu vilevile.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις