Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




2 Samweli 4:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Mutu mwovu anapomwua mutu wa haki akiwa katika kitanda ndani ya nyumba yake, basi si ni jambo la haki kwangu kumulipiza kwa sababu ya kumwanga damu kwa kumwondosha toka katika dunia?”

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




2 Samweli 4:11
19 Σταυροειδείς Αναφορές  

Sasa wewe unalaaniwa juu ya udongo ambao ulifungua kinywa kwa kupokea damu ya ndugu yako uliyemwua.


Mungu akamwambia Noa: “Nimeamua kuwaangamiza wanadamu wote kwa sababu wamejaza dunia mateso makali. Hakika, nitawaangamiza kabisa pamoja na dunia!


Mungu akaangamiza kila kiumbe kilichokuwa na pumzi ya uzima katika dunia: wanadamu, nyama, viumbe vinavyotambaa na ndege wa anga. Vyote viliangamizwa katika dunia. Noa tu ndiye aliyebaki na wale waliokuwa pamoja naye ndani ya chombo.


Yawe amekulipiza kisasi kutokana na kumwanga damu ya watu wote wa jamaa ya Saulo, ambaye sasa wewe umenyanganya ufalme kwa pahali pake. Sasa, Yawe amemupa mwana wako Abusaloma ufalme. Maangamizi yamekupata kwa sababu wewe ni mwuaji.”


Abeneri aliporudi Hebroni, Yoabu alimupeleka pembeni kwenye mulango sawa vile anataka kuzungumuza naye kwa siri. Hapo Yoabu akamukata Abeneri katika tumbo kwa sababu Abeneri alikuwa amemwua ndugu yake Asaeli, na Abeneri akakufa.


Ijapokuwa mumenipakaa mafuta kusudi nikuwe mufalme, lakini leo mimi ni zaifu. Hawa wana wa Zeruya ni wakali kupita kipimo. Yawe awaazibu waovu hawa sawasawa na uovu wao.”


Mungu atamwazibu Yoabu kwa mauaji hayo aliyoyafanya bila baba yangu kuwa na habari. Yeye aliwaua watu wawili ambao walikuwa wa maana zaidi kuliko yeye, tena walimupita kwa wema; aliwaua Abeneri mwana wa Neri, jemadari wa kundi la waaskari Waisraeli, na Amasa mwana wa Yeteri, jemadari wa waaskari wa Yuda.


Yawe akumbuke zambi zao siku zote; lakini wao wenyewe wasahauliwe katika dunia.


Mumwimbie sifa Yawe anayekaa Sayuni! Muyatangazie mataifa mambo aliyotenda!


Anayepiga mutu na kumwua, hakika anapaswa kuuawa.


Ningalikwisha kukuangamiza wewe na watu wako kwa ugonjwa mukali, nanyi mungalikuwa mumekwisha kuangamia.


Lakini waovu wataondolewa katika inchi, na watu wabaya watangolewa toka ndani yake.


Mwenye haki anayekubali kufuata mambo ya mwovu ni chemichemi iliyochafuliwa au kisima kinachotofuliwa.


Basi, utawaambia hivi: Miungu hiyo ambayo haikuumba mbingu na dunia itaangamia. Itatoweka kabisa toka katika dunia, hapa chini ya mbingu.


Wewe si ndiwe Yawe, tangu zamani sana? Wewe ndiwe Mungu wangu, Mutakatifu wangu, usiyekufa. Ee Yawe, umewachagua Wakaldea watuhukumu! Ewe kimbilio letu, umewaimarisha kusudi watuazibu!


Hivyo sheria haina nguvu, wala haki haifuatiliwi. Waovu wanawazunguka wenye haki, hivyo hukumu inatolewa na sheria imepotoshwa.


Tusikuwe kama Kaina aliyekuwa wa yule Mwovu, akamwua ndugu yake. Yeye alimwua kwa sababu gani? Kwa sababu matendo yake yalikuwa mabaya na ya ndugu yake yalikuwa ya haki.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις